KATIKA kuhakikisha kuwa msikilizaji wa Efm kupitia kipindi chake cha Joto la Asubuhi anapata taarifa za kutosha na zilizosheheni masuala mbalimbali ya Kijamii, kuanzia Juni 29, Jumatatu, kitakuwa na habari kutoka mikoa mbalimbali nchini katika kipengele cha kona zote.
Msimamizi Mkuu wa Kipindi hicho Dennis Ssebo ameitonya Blog ya Jamii kuwa tofauti na utaratibu wa kuripoti matukio uliozoeleka Joto la asubuhi litakuwa likizimulika na kuzichambua habari hizo zilizoandikwa na wabobezi wa mambo katika tasnia ya habari kuanzia saa kumi na mbili hadi saa kumi na mbili na nusu asubuhi.
Joto la asubuhi ni kipindi cha asubuhi ambacho kinaruka hewani kupitia 93.7 EFM kila siku Jumatatu hadi Ijumaa kuanzia saa kumi na mbili hadi saa tatu kamili asubuhi chini ya watangazaji wake mahili Dennis Ssebo na Adella Tillya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...