BARAZA la Mchele nchini (RCT) kwa kushirikiana na taasisi isiyo ya kiserikali inayojihusisha na masuala ya kilimo (ANSAF), wameishauri serikali kutekeleza na kuendeleza sheria ya tozo ya ushuru wa forodha ya asilimia 75 kwa mchele unaotoka nje ya Shirikisho la Afrika Mashariki ili kuwaboreshea bei wakulima wa hapa nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kwenye mkutano wa kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabili wakulima wa mchele, Mkurugenzi Mtendaji wa Ansaf, Audax Rukonge, alisema kwa kufanya hivyo kutasaidia mkulima wa hapa nchini aweze kupata bei inayoendana na uhalisia wa zao hilo.

Rukonge alisema mchele mwingi unaoingizwa hapa nchini umekuwa haulipiwi kodi, jambo linalosababisha madhara makubwa kwa mkulima, ikiwemo kushindwa kujiendeleza katika kilimo hicho na kuongeza kwamba kwa sasa mawaziri wa shirikisho hilo wapo mbioni kutaka kubadilisha ushuru huo uwe chini ya asilmia 75, jambo ambalo halikubaliki.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Mchele Tanzania (RCT), Julius Wambura, alisema serikali inatakiwa kupanua wigo wa ukusanyaji wa takwimu za bei ya mchele ili kila mwananchi aweze kupata taarifa sahihi na kwa wakati.


Kama vile haitoshi, Wambura aliomba serikali kuwezesha bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko ianze kazi ili iweze kutekeleza majukumu yake pamoja na kuweka madaraja na viwango vya ubora vinavyotakiwa kwa walaji wa mchele wa ndani na masoko ya nje.
Mkurugenzi Mtendaji wa Ansaf, Audax Rukonge akizungumza na waandishi wa habairi jijini Dar es Salaam, kwenye mkutano wa kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabili wakulima wa mchele,
Mwenyekiti wa Baraza la Mchele Tanzania, Julius wambura akifungua semina  hiyo
Mkurugenzi Mtendaji wa Ansaf, Audax Rukonge akizungumza na waandishi wa habairi jijini Dar es Salaam, kwenye mkutano wa kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabili wakulima wa mchele.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...