BARAZA
la Mchele nchini (RCT) kwa kushirikiana na taasisi isiyo ya kiserikali
inayojihusisha na masuala ya kilimo (ANSAF), wameishauri serikali kutekeleza na
kuendeleza sheria ya tozo ya ushuru wa forodha ya asilimia 75 kwa mchele
unaotoka nje ya Shirikisho la Afrika Mashariki ili kuwaboreshea bei wakulima wa
hapa nchini.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kwenye mkutano wa kujadili
changamoto mbalimbali zinazowakabili wakulima wa mchele, Mkurugenzi Mtendaji wa
Ansaf, Audax Rukonge, alisema kwa kufanya hivyo kutasaidia mkulima wa hapa
nchini aweze kupata bei inayoendana na uhalisia wa zao hilo.
Rukonge
alisema mchele mwingi unaoingizwa hapa nchini umekuwa haulipiwi kodi, jambo
linalosababisha madhara makubwa kwa mkulima, ikiwemo kushindwa kujiendeleza
katika kilimo hicho na kuongeza kwamba kwa sasa mawaziri wa shirikisho hilo
wapo mbioni kutaka kubadilisha ushuru huo uwe chini ya asilmia 75, jambo ambalo
halikubaliki.
Naye
Mwenyekiti wa Baraza la Mchele Tanzania (RCT), Julius Wambura, alisema serikali
inatakiwa kupanua wigo wa ukusanyaji wa takwimu za bei ya mchele ili kila
mwananchi aweze kupata taarifa sahihi na kwa wakati.
Kama
vile haitoshi, Wambura aliomba serikali kuwezesha bodi ya nafaka na mazao
mchanganyiko ianze kazi ili iweze kutekeleza majukumu yake pamoja na kuweka
madaraja na viwango vya ubora vinavyotakiwa kwa walaji wa mchele wa ndani na
masoko ya nje.
Mkurugenzi Mtendaji wa Ansaf, Audax Rukonge akizungumza na waandishi wa habairi jijini Dar es Salaam, kwenye mkutano wa kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabili wakulima wa mchele,
Mwenyekiti wa Baraza la Mchele Tanzania, Julius wambura akifungua semina hiyo
Mkurugenzi Mtendaji wa Ansaf, Audax Rukonge akizungumza na waandishi wa habairi jijini Dar es Salaam, kwenye mkutano wa kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabili wakulima wa mchele.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...