Balozi, Patrick Chokala akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutangaza nia ya kugombea nafasi ya Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi(CCM) leo katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda,
Globu ya Jamii
Mwandishi wa Habari wa Rais wa awamu ya Pili, BaloziPatrick Chokala ametangaza nia ya kugombea urais ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ili aweze kupeperusha bendera hiyo katika uchaguzi mkuu ujao mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari leo katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jijini Dar es Salaam, Balozi Chokala amesema umefika wakati wa kurejesha haki kwa wananchi ili wawe na imani na uongozi na pia kuwa na ari ya kuleta maendeleo.
Amesema katika kutekeleza miradi inapaswa kutumia watalaam wa elimu ya jamii kikamilifu kabla ya kutekeleza kama mradi wa gesi ambao ilileta vurugu katika mikoa ya Kusini wakati serikali ilikuwa ina nafasi ya kuelewesha wananchi.
“Nimekuwa na uzoefu wa kutosha kuwafahamu watanzania kwa miaka 13 nimekuwa Ikulu na pia nchi za nje nilizofanya kazi mfano Nigeria na Urusi”amesema Balozi Chokala.
Chokala atakuwa ni mtu wa 38 kama atachukua fomu katika kinyanganyiro cha urais katika Chama cha Mapinduzi (CCM).
Wakati wengine wanatangaza nia zao baadhi ya wagombea katika nafasi hiyo ya CCM wanamaliza kutafuta wadhamini katika mikoa mbalimbali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...