Wadau wa benki ya NMB pamoja na wageni waalikwa wakisikiliza kwa umakini hotuba ya mgeni rasmi ambaye alikuwa ni Rais mstaafu wa awamu ya tatu Mhe. Benjamin William Mkapa wakati wa uzinduzi wa huduma mpya ya MasterCard itakayoanza kutumiwa rasmi na benki hiyo. Uzinduzi huo ulifanyika katika Hoteli ya Haytt Regency zamani Kilimanjaro, jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Master Card kanda ya Afrika ya kati, Bw. Michael Mieback, akiwahutubia wadau wa Benki ya NMB wakati wa hafla ya uzinduzi wa kadi hiyo mpya ambayo itaanza kutumiwa rasmi na benki hiyo. Hafla hiyo ilifanyika katika hoteli ya Haytt Regency zamani Kilimanjaro jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa bodi, benki ya NMB, Prof. Joseph Semboja (kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi mkuu wa Benki hiyo, Bi. Ineke Bussemaker (katikati) wakati wa uzinduzi wa huduma mpya ya MasterCard iliyozinduliwa rasmi na benki hiyo katika hotel ya Hyatt Regency jijini Dar es salaam. (Kulia) ni Afisa wa Master Card kanda ya Afrika ya kati Bw. Michael Mieback aliyehudhuria mkutano huo.
  Mwenyekiti wa bodi benki ya NMB, Prof. Joseph Semboja (kushoto), Mkurugenzi mkuu wa Benki ya NMB Bi. Ineke Bussemaker (katikati) pamoja na Rais wa Master Card kanda ya Afrika ya kati, Bw. Michael Mieback, (kulia) wakiteta jambo kabla ya uzinduzi wa huduma mpya ya MasterCard itakayoanza kutumika katika benki hiyo. Hafla hiyo ilifanyika katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...