Na mwandishi wetu.
Washiriki wa
mbio za baiskeli zijulikanazo kama “Acacia Tufanikiwe Pamoja Lake Zone
Cycle Challenge” kutoka mikoa ya Shinyanga na Mwanza wameendelea
kuudhihirisha umma wa wakazi wa kanda ya ziwa na watanzania kwa ujumla kuwa
mpaka sasa hawana mpinzani baada ya washiriki wa mbio hizo kuibuka kidedea
katika fainali za kumtafuta mshindi wa kanda hiyo.
Washiriki wa
mikoa hii miwili wamejinyakulia nafasi zote za juu na hivyo kuwashinda wenzao
wa mikoa mingine ya Kanda ya ziwa ikiwemo Kagera, Mara, Geita na Simiyu.
Katika mbio
za wanaume za umbali wa kilometa 156.6 kutoka Kahama mpaka Tinde na kisha
Kurejea Kahama, mshindi wa mwaka jana Masunga Duba (Mwanza) aliibuka tena
kidedea huku nafasi ya pili ikichukuliwa na Lupilya Hamis(Shinyanga) na nafasi
ya tatu ikimuendea Kulwa Tuki(Shinyanga), washindi hawa wamejinyakulia kitita
cha pesa taslimu Sh1,500.000/- kwa mshindi wa kwanza, Sh1,200.000/= mshindi wa
pili na Sh800,000/= kwa mshindi wa tatu.
Kwa upande
wa mbio za wanawake za umbali wa kilometa 80, kutoka Kahama mpaka Mwakata Kisha
kurejea Kahama, timu ya mkoa wa Mwanza imedhihirisha kuwa wao bado ni mabingwa
kwa kuibuka tena washindi wa mbio hizo, huku mshindi wa mbio za Mwaka jana
Martha Antony, akiibuka mshindi wa kwanza akifuatiwa na Laulensia Luziba na
nafasi ya tatu ikienda kwa Veronica Simon. Washindi hao wamepata zawadi ya pesa
taslimu Sh1,200.000/= kwa mshindi wa kwanza, Sh800,000/= mshindi wa pili na
Sh600,000/= mshindi wa tatu.
Mshindi wa mbio za Acacia Tufanikiwe Pamoja Lake Zone Cycle Challenge, Masunga Duba aliyeinua mikono akishangilia mara baada ya kumaliza mbio hizo akiwa mbele ya wenzake. Mshindi huyo anatoka mkoa wa Shinyanga.
Washindi wa mbio za wanawake (kilometa 80). Aliyesimama katikati ni Martha antony ambaye ndio aliibuka mshindi wa kwanza, akifuatiwa na Laulensia Luzuba, (mwenye mtoto) aliyekuwa mshindi wa pili na Veronica Saimon (wa kwanza kushoto) aliyejinyakulia nafasi ya Tatu.
Baiskeli ya kwanza ya kisasa inagia zingine swala kichekesho
ReplyDelete