Baadhi ya Washiriki wa Kongamano la kukaribisha mwezi mtukufu wa Ramadhan wakibadilishana mawazo nje ya Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere kabla ya Kuingia Ndani ya Ukumbi  huo ili kujadili Kauli Mbiu ya Ndoa Chanzo Cha Utu wetu Jana 14.06.2015.
 Baadhi ya wataalamu wa Kiislam wakimsilizi kwa Makini Dr Ahmad Totonji Kutoka Suadi Arabia alipokuwa akiwakilisha Mada ya Taasisi ya Ndoa, Jana, leo na Kesho Katika Kongamano la Kukaribisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Dr. Totonji  amewasihi waislam wataalamu kuwa chachu ya mfano wa Ndoa Imara katika Jamii.
  Dr. Ahmed Totonji (Mwenye Kanzu) akiteta Jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Amana Banki Dr. Muhsin Muhsin wakati wa Kongamano la wataalamu wa Kiislam la Kukaribisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani unaotegemewa kuanza katikati ya wiki hii.
 Mh. Asha Mtwangi akichangia Mawazo juu ya Kauli Mbiu ya Kongamano la Kukaribisha Mwezi wa Ramadhan ambayo ilikuwa Ndoa Chanzo Cha Utu wetu ambalo mada ya Taasisi ya Ndoa: Jana, Leo na Kesho pamoja na Familia katika Changamoto ya utandawazi. Mh. Asha Mtwangi alihamasisha taasisi mbali mbali kuweka nguvu zaidi kuwapa mafunzo ya dini vijana na wanandoa ili kuhakikisha wanafahamu majukumu sahihi ndani ya ndoa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 15, 2015

    Kwa wale ambao tulishindwa kuhudhuria kongamano hilo, tutapataje nakala za mada zilizotolewa katika kongamano hilo??

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...