Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwasili kwenye Uwanja wa wa Ndege wa Kimataifa wa Sharm El Sheikh, jijini Sharm El Sheikh Cairo Misri, kwa ajili ya kuhudhuri Mkutano Mkuu wa tatu wa Wakuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Soko la pamoja la nchi za Kusini mwa Afrika (COMESA) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Waziri wa Uchukuzi wa Egypt, Hossam Kamal, wakati alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Sharm El Sheikh, jijini Sharm El Sheikh Cairo Misri, kwa ajili ya kuhudhuri Mkutano Mkuu wa tatu wa Wakuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Soko la pamoja la nchi za Kusini mwa Afrika (COMESA) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC). Agenda ya mkutano huo ni kupokea taarifa ya majadiliano ya kuanzisha eneo huru la Biashara la Utatu wa EAC, COMESA na SADC.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Waziri wa Afrika Mashariki, Dkt. Harrison Mwakyembe, wakati alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Sharm El Sheikh, jijini Sharm El Sheikh Cairo Misri, kwa ajili ya kuhudhuri Mkutano Mkuu wa tatu wa Wakuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Soko la pamoja la nchi za Kusini mwa Afrika (COMESA) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Waziri wa Uchukuzi wa Egypt, Hossam Kamal, kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Sharm El Sheikh, jijini Sharm El Sheikh Cairo Misri. Dkt. Bilal, amewasili Jijini Sharm El Sheikh kwa ajili ya kuhudhuri Mkutano Mkuu wa tatu wa Wakuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Soko la pamoja la nchi za Kusini mwa Afrika (COMESA) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC). Picha na OMR
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...