Meneja Mradi wa Sports Development Aid (SDA) Bw. Mohamed Chigogolo akielezea jambo wakati wa hafla ya kuwaaga watoto wanaoenda kushiriki michuano ya Kombe la Helsinki nchini Finland, hafla hiyo imefanyika jana katika ukumbi wa Ubalozi wa Finland jijini Dar es Salaam.Katikati ni Afisa Michezo Mwandamizi kutoka Wizara ya Habari, Vijana, na Michezo Bw. Nicholaus Bulamile na Kaimu Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Bw. Boniface Wambura.
 Balozi wa Finland nchini Bibi. Sinikka Antila akipeana mkono wa mmoja wa wachezaji wa timu ya Vito FC ya wilayani Kilwa mkoa wa Lindi wakati wakiagwa kwa ajili ya kuelekea nchini Finland jana jijini Dar es Salaam. Timu hiyo inaelekea nchini humo kushiriki mashindano ya Kombe la Helsinki ambayo yanahusisha jumla ya timu za watoto walio na umri chini ya miaka 12.Mshindano hayo yanatarajiwa kuanza tarehe 05 Julai 2015 na kushirikisha zaidi ya timu 1000. 
 Balozi wa Finland nchini Tanzania Bibi. Sinikka Antila akipngea  na wachezaji wa Timu ya VITO FC kutoka Kilwa mkoani Lindi, ambayo ilikuwa inaagwa kabla ya kuelekea nchini Finland kwa ajili ya kushiriki michuano ya Kombe la Helsinki itakayoanza kutimua vumbi tarehe 05 Julai jijini Helsinki Finland. Timu hiyo imepata ushiriki huo kupitia Asasi ya kirai ya Sports Development Aid (SDA) ikiwa na lengo la kutumia michezo kama nyenzo ya kuhamasisha jamii kuwapeleka watoto wao wakapate elimu.
 Balozi wa Finland nchini Bibi. Sinikka Antila akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya Vito FC ya Kilwa mkoani Lindi wakati wa hafla ya kuwaga kwa ajili ya kuelekea nchini Finland jana jijini Dar es Salaam. Timu hiyo inaelekea nchini humo kushiriki mashindano ya Kombe la Helsinki ambayo yanahusisha jumla ya timu za watoto walio na umri chini ya miaka 12.Mshindano hayo yanatarajiwa kuanza tarehe 05 Julai 2015 na kushirikisha zaidi ya timu 1000.

Kaimu Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Bw. Boniface Wambura akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya Vito FC ya Kilwa mkoani Lindi wakati wa hafla ya kuwaga kwa ajili ya kuelekea nchini Finland jana jijini Dar es Salaam. Timu hiyo inaelekea nchini humo kushiriki mashindano ya Kombe la Helsinki ambayo yanahusisha jumla ya timu za watoto walio na umri chini ya miaka 12.Mshindano hayo yanatarajiwa kuanza tarehe 05 Julai 2015 na kushirikisha zaidi ya timu 1000.

Picha na Frank Shija, WHVUM

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...