Bi Moza akiwa  akimshindikiza 
mtoto wake Moh'd Saidi, 
Nchini India kwa matibabu
Bi Moza Moh'd Khamis anapenda tena kutoa shukurani za dhati kwa wale wote waliochangia kwa hali na mali kwa mtoto wake Moh'd Said Moh'd,  kwenda kufanyiwa matibabu ya upandikizaji wa figo, nchini India.

Mapema asubuhi ya leo Bi Moza aliongea na blog ya swahilivilla ili kutoa taarifa kwa kukamilika safari yake ya kwenda nchini India pamoja na kutaka tumuombe Dua za kumtakia kila la kheri  katika safari hiyo.

Moh'd Said Moh'd ameondoka leo Jumanne Juni 9, katika  uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam kuelekea Nchini India kwaajili ya matibabu yake.

Napenda kuchukua fursa hii kwa niaba ya Tanzania Bloggers Network (DMV) na waTanzania wote waishio Nchini Marekani, kumtakia kila la kheri  Ndugu yetu Moh'd Said Moh'd katika matibabu yake huko Nchini India.

M/Mungu amjaalie wepesi katika safari yake na ampe afuweni na mafanikio katika mipangilio yote matibabu yake. Ameen.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...