Na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.
JENGO la ghorofa 16 lililopo mtaa wa Indira Ghandi jijini Dar es Salaam linatarajiwa kubomolewa kwa kuwa linadaiwa kujengwa chini ya kiwango.

 Amri hiyo imetolewa na  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiki wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam,amesema kuwa uwepo wa jengo hilo ambalo limejengwa chini ya kiwango limezua hofu kubwa kwa wakazi wa eneo hilo,kwani jengo hilo lipo karibu na jengo lingine lililokuwa na ghorofa 16 ambalo lilianguka wakati wa ujenzi wa ghorofa hilo ukiendelea.

Hatua za ubomoaji  wa jengo hilo zinaendelea wakati wakazi wa eneo hilo  wameombwa kuepuka na madhara yatakayojitokeza katika ubomoaji wa jengo hilo.

Kampuni ambayo imepewa dhamana ya ubomoaji wa Jengo hilo ni  kampuni ya  Kichina ya ERJE ambayo wanasubiri itekeleze wajibu wake katika kubomoa jengo hilo.
Jengo la Ghorofa 16 ambalo linatakiwa kubomolewa lililopo katika mtaa wa Indira Ghadhi jijini Dar es Salaam.(Picha na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 04, 2015

    Linabomolewa kwa sababu ya wasiwasi tu wa wakazi wa eneo hilo au wataalamu wamepima na kuona kuwa liko chini ya kiwango?!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...