Marehemu alizaliwa mwaka 1944 katika kijiji cha Kidia, Old Moshi, Mkoa wa Kilimanjaro.  Alipata elimu ya msingi katika Shule ya Msingi Kidia mwaka 1951 – 1954 na baadae Shule ya Msingi Kidia Juu (Kidia Upper Primary School) mwaka1955 – 1958.   
 Alihitimu Elimu ya Sekondari Kidato cha Nne mwaka 1974 katika Shule ya Sekondari Mawenzi akiwa mtahiniwa wa kujitegemea (Private Candate). Aidha, alisoma Cheti cha Sheria Chuo Kikuu cha D’Salaam mwaka 1975 – 1976 na baadaye Shahada ya Kwanza ya Sheria Chuo Kikuu cha D’Salaam mwaka 1977 – 1980. 

Marehemu ajiunga na Jeshi la Magereza mwaka 1964 baada ya kuhitimu Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza Chuo Ukonga, D’Salaam yaliyofanyika kuanzia Januari - Julai, 1964.  Ndani ya utumishi, alipata fursa ya kuhudhuria Mafunzo ya Uongozi Daraja la Pili (Advance Course) Chuo Ukonga, D’Salaam kuanzia Aprili – Julai, 1967 na Mafunzo ya Uongozi wa Juu (Gazetted Course) kuanzia Februari – Mei, 1974.

Kutokana na utendaji wake wa kazi, marehemu aliwahi kutunukiwa vyeo mbalimbali kama ifuatavyo:-

·        Afisa Magereza Daraja la Tatu mwaka 1964
·        Afisa Magereza Daraja la Pili mwaka 1965
·        Afisa Magereza Mkuu Daraja la Nne mwaka 1967
·        Afisa Magereza Mkuu Daraja la Tatu mwaka 1971
·        Mrakibu Msaidizi wa Magereza mwaka 1975
·        Mrakibu wa Magereza mwaka 1976
·        Mrakibu Mwandamizi wa Magereza mwaka 1978
·        Kamishna Msaidizi wa Magereza mwaka 1982
·        Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza mwaka 1984
·        Kamishna wa Magereza mwaka 1992
·        Kamishna Mkuu wa Magereza mwaka 1996 – 2002

HABARI ZAIDI INGIA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...