Marehemu alizaliwa mwaka 1944 katika kijiji cha
Kidia, Old Moshi, Mkoa wa Kilimanjaro.
Alipata elimu ya msingi katika Shule ya Msingi Kidia mwaka 1951 – 1954 na
baadae Shule ya Msingi Kidia Juu (Kidia Upper Primary School) mwaka1955 –
1958.
Alihitimu Elimu ya Sekondari
Kidato cha Nne mwaka 1974 katika Shule ya Sekondari Mawenzi akiwa mtahiniwa wa
kujitegemea (Private Candate). Aidha, alisoma Cheti cha Sheria Chuo Kikuu cha
D’Salaam mwaka 1975 – 1976 na baadaye Shahada ya Kwanza ya Sheria Chuo Kikuu
cha D’Salaam mwaka 1977 – 1980.
Marehemu ajiunga na Jeshi la Magereza mwaka 1964
baada ya kuhitimu Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza Chuo Ukonga, D’Salaam
yaliyofanyika kuanzia Januari - Julai, 1964.
Ndani ya utumishi, alipata fursa ya kuhudhuria Mafunzo ya Uongozi Daraja
la Pili (Advance Course) Chuo Ukonga, D’Salaam kuanzia Aprili – Julai, 1967 na
Mafunzo ya Uongozi wa Juu (Gazetted Course) kuanzia Februari – Mei, 1974.
Kutokana na utendaji wake wa kazi, marehemu
aliwahi kutunukiwa vyeo mbalimbali kama ifuatavyo:-
·
Afisa Magereza Daraja la Tatu mwaka 1964
·
Afisa Magereza Daraja la Pili mwaka 1965
·
Afisa Magereza Mkuu Daraja la Nne mwaka
1967
·
Afisa Magereza Mkuu Daraja la Tatu
mwaka 1971
·
Mrakibu Msaidizi wa Magereza mwaka
1975
·
Mrakibu wa Magereza mwaka 1976
·
Mrakibu Mwandamizi wa Magereza mwaka
1978
·
Kamishna Msaidizi wa Magereza mwaka
1982
·
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa
Magereza mwaka 1984
·
Kamishna wa Magereza mwaka 1992
·
Kamishna Mkuu wa Magereza mwaka 1996 –
2002
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...