Katibu
Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia katika mkutano wa
hadhara wa kuhitimisha ziara ya miezi 26 katika mikoa 31 nchini, ya
kuimarisha uhai wa chama, kukagua, kuhimiza na kusimamia Utekelezaji wa
Ilani ya Uchaguzi ya CCM, pamoja na kusikiliza kero za wananchi na
kuzitafutia ufumbuzi.
Mkutano
huo umefanyika kwenye viwanja vya Furahisha, Kirumba jijini Mwanza jana jioni. Ndugu Kinana ambaye katika ziara hiyo ameambatana na
Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, tayari wamesafiri umbali wa Km
193,537, kwa kufika katika Wilaya 163, majimbo 239, nusu ya vijiji na
kata 1938 za Tanzania. Pia msafara wake ulitumia jumla ya saa 84
kuzunguka mikoa yote hiyo, na kusafiri kwa mitumbwi katika visiwa 16.
Amehutubia jumla ya mikutano ya ndani/hadhara 1918 na kujikusanyia
wanachama wapya 284300 ambapo kutoka upinzani 38984.
Aliyekuwa
mgombea wa ubunge kwa tiketi ya Chadema, katika uchaguzi mkuu uliopita,
Twalib Ngika, akikabidhi Kadi ya Chadema kwa Katibu Mkuu wa CCM,
Abdulrahman Kinana baada ya kutangaza kuhamia CCM, wakati wa mkutano wa
hadhara wa Katibu Mkuu huyo uliofanyika viwanja vya Furahisha jijini
Mwanza jana.
Katibu
wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, akihutubia katika mkutano wa
hadhara kwenye Uwanja wa Furahisha jijini Mwanza jana jioni, ambapo amewataka
viongozi wa chama na Serikali kutoka maofisini kwenda kwa wananchi
kuzitafutia ufumbuzi kero zao.
Katibu
Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana akifafanua jambo mbele ya wakazi
wa jiji la Mwanza na vitongoji vyake,alipokuwa akiwahutubia katika
mkutano wa hadhara wa kuhitimisha ziara ya miezi 26 katika mikoa 31
nchini, ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua, kuhimiza na kusimamia
Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM, pamoja na kusikiliza kero za
wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akiagana na wananchi mara baada ya kumaliza
kuwahutubia kwenye Uwanja wa Furahisha jijini Mwanza jioni ya leo,Kinana
aliwahutubia wananchi na kuahidi kuwa bunge lijalo kwa upande wa CCM,
litakuwa na mabadiliko makubwa kwa kuwapa nguvu wabunge kuihoji serikali
kuhusu utendaji wake.
Ndugu
Kinana akiwapungia mkono wananchi alipokuwa wakiwasili kwenye Uwanja wa
Furahisha jijini Mwanza, ambapo aliwahutubia wananchi na kuahidi kuwa
bunge lijalo kwa upande wa CCM, litakuwa na mabadiliko makubwa kwa
kuwapa nguvu wabunge kuihoji serikali kuhusu utendaji wake.
Sehemu ya umati wa watu waliohudhuria mkutano wa CCM kwenye Uwanja wa Furahisha jijini Mwanza jana.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...