Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikaribishwa  na Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini CGP John Casmir Minja  katika Viwanja vya Chuo cha Maafisa Magereza, Ukonga jijini Dar es Salaam Jumamosi, kuhudhuria Siku ya MAgereza na  kufunga mafunzo ya uofisa wa Cheo cha Mrakibu Msaidizi wa Jeshi hilo. Maafisa 104 wa kozi hiyo walihitimu mafunzo hayo na kuvishwa vyeo hivyo. Kulia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe.
 Rais Jakaya Kikwete akikagua gwaride liloandaliwa kwa ajili yake na wahitimu wa Mafunzo ya Uongozi wa Ngazi za Juu wa Jeshi la Magereza kabla ya kuyafunga mafunzo ya Cheo cha Mrakibu Msaidizi yaliyofanyika katika viwanja vya Chuo cha Maafisa wa Jeshi hilo, Ukonga jijini Dar es Salaam. Rais Kikwete aliyafunga mafunzo hayo ambayo yalienda sambamba na Siku ya Magereza ambapo alikagua bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na jeshi hilo nchini.
 Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Kikwete akimvisha mhitimu Amina Lidenge, Cheo cha Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Magereza kwa niaba ya wenzake 104 waliomaliza mafunzo hayo katika Chuo cha Maafisa wa Jeshi hilo, Ukonga jijini Dar es Salaam.
Gwaride la Wahitimu wa mafunzo ya uofisa wa Cheo cha Mrakibu Msaidizi wa Jeshi hilo.
 Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri Chikawe  na Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini CGP John Casmir Minja wakiwa na Makamishna Jenerali wastaafu. Kutoka Kulia ni Augustine Nanyaro, Nicas Banzi, CGP John Minja, Rais Kikwete, Alhaj Jumanne Mangara, Simon Mwanguku, na Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Mathias Mathias Chikawe.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...