Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitembelea shamba la ndizi na kahawa la  mkulima wa Kahawa na Ndizi Ndugu Eustace Kubalienda Kishunji katika kijiji cha Mabila,wilayani Kyerwa mkoani Kagera
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo kutoka kwa mkulima wa Kahawa na Ndizi Ndugu Eustace Kubalienda Kishunji ambaye ni mmiliki wa shamba la Ndizi,, Amesema shamba hilo  lina  miche 345 ambayo huvuna magunia 25 na ana shamba la migomba ambalo humpatia mavuno ya  mikungu  kwa mwezi 45.

Mzee Kishunji ambaye anaishi katika kijiji cha Kikukuru kata ya Mabira ameweza kusomesha watoto wawili katika vyuo vikuu vya Dar es salaam na Dodoma na amejenga nyumba ya kisasa yenye thamani kubwa ya fedha kutokana na kilimo bora cha kisasa.

Katibu Mkuu Kinana yuko ziarani katika mikoa ya Kagera , Geita na Mwanza akikagua utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010, akiongozana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye
 Mkulima bora wa migomba na kahawa katika Kijiji cha Mabira, Mzee Eustus kishunju Ntibalienda (kulia) akimpatia maelezo Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, kuhusu alivyoweza kufanikiwa katika kilimo cha mazao hayo, Katibu Mkuu alipomtembelea mkulima huyo,  akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM na Uhai wa Chama katika wilaya ya Kyerwa, mkoani Kagera, leo. 
 Sehemu ya soko la biashara la kisasa na la kimataifa linalojengwa Kigorogoro,mpakani mwa Tanzania na Uganda.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (pichani kati) akiwa ameongozana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye pamoja na Mkuu wa mkoa wa Kagera Mh.John Mongella wakijadiliana jambo mara baada ya kuzungumza na wananchi wa Kijiji cha Kigorogoro, alipowasili katika kijiji hicho kukagua ujenzi wa soko la kisasa na la Kimataifa katika kijiji hicho leo.

Hhata hivyo Kinana ameonesha kusikitishwa baada ya kujulishwa kuwa ujenzi wa mradi huo, unaohitaji sh. bilioni 1.5 umesimama kutokana na serikali kuu kukosa fedha.

        Kutokana na hali hiyo, Katibu Mkuu wa CCM, amesema ni vema miradi muhimu ya maendeleo iwekwe chini ya usimamizi wa halmashauri ya eneo linalohusika badala ya serikali kuu. 

       Amesema, utaratibu wa kuifanya miradi ya aina hiyo kuwa chini ya usimamizi wa serikali, umekuwa ukileta matokeo mabaya ikiwemo kusimama kwa ujenzi wa miradi.

       Kinana amesema hayo leo, baada ya kukagua ujenzi wa kitu kikubwa cha biashara, katika Kata ya... wilayani Kerwa mkoa ni Kagera ambacho ujenzi wake umesimama tangu mwaka juzi kwa maelezo ya kukosekana fedha.

      "Jamani jengo kama hili lilitakiwa lisimamiwe na Halmashauri ya eneo hili, lakini kusimamiwa na wizara ni kupoteza muda, hivi kweli ni rahisi mkaguzi atoke Dar es Salaam, kuja hadi huku kukagua ujenzi tu wa jengo hili, hasa ikizingatiwa kuwa miradi kama hii ni mingi?" alihoji Kinana.
 Wananchi wa Kijiji cha Kigorogoro katika Kata ya Murongo wilayani Kyerwa mkoani Kagera wakimshangilia Katibu Mkuu wa CCm, Abdulrahman Kinana akipowasili kuwahutubia mkutano wa hadhara katika kijiji hicho leo.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akiwahutubia Wananchi wa kijiji cha Kibingo Wilayani kyerwa mkoani Kagera.
 Wananchi wa kijiji cha Isingiro wakimshangilia Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi,alipopanda jukwaani na kuwasalimia.
 Wananchi wa kijiji cha Isingiro wakimsikiliza Katibu Mku wa CCM,Ndgu Kinana alipokuwa akiwahutubia.

PICHA NA MICHUZI JR-KYERWA KAGERA.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Tunashukuru kwa ushauri mzuri wa Mh: Kinana, japo bado hata hao Halmashauri wakiachiwa kusimamia miradi nao ni sehemu ya serikali, bado Luna tatizo la watendaji wetu kutokuwa na mapenzi mema kwa nchi yao.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...