Mhe. Hussein Kattanga, Mtendaji Mkuu, Mahakama ya Tanzania (wa kwanza kushoto), Bw. Waleed Malik, Mwakilishi kutoka Benki ya Dunia (wa pili kushoto), Bi. Neema Ndunguru, Mkurugenzi wa Mazingira ya Biashara (PDB) pamoja na wawakilishi kutoka Benki ya Dunia wakiwa meza kuu wakati wa Kikao cha majadiliano katika ya Mahakama na Wadau wa Jumuiya ya Wafanyabiashara kupata maoni juu ya maboresho ya huduma za Mahakama. (IMG. 7436)
 Mmoja wa wadau walioshiriki katika warsha hiyo akitoa maoni yake katika majadiliano hayo. (IMG. 7449)
 Washiriki wakiwa katika kazi za makundi wakitoa maoni juu ya Mpango Mkakati wa Mahakama wenye lengo la kuboresha utoaji wa huduma zake.  (IMG. 7465) (Picha na Mary Gwera, Mahakama)

Na Mary Gwera
KATIKA mwendelezo wa maboresho ya utoaji wa huduma ya haki nchini, Mahakama ya Tanzania inaendelea kufanya jitihada mbalimbali ikiwa ni pamoja na kukutana na wadau pamoja na Washirika mbalimbali wa maendeleo ili kupata maoni yao juu ya uboreshaji wa huduma zake.
Akiongea na Waandishi wa Habari mapema jana, katika Warsha iliyoandaliwa na  Mahakama ikishirikisha Ugeni kutoka Benki ya Dunia na Wawakilishi kutoka Jumuiya ya Wafanyabiashara kutoka, TRA, Umoja wa Taasisi za Kifedha,MOAT, TIRA, TCRA n.k iliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Hyatt jijini Dar es Salaam, Bw. Hussein Kattanga, Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania alisema Mahakama imekuwa katika mchakato wa maboresho na washirika mbalimbali wa Maendeleo na wadau wa utoaji haki ili kuboresha huduma zake.

KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...