Mhe. Hussein Kattanga, Mtendaji Mkuu, Mahakama ya
Tanzania (wa kwanza kushoto), Bw. Waleed Malik, Mwakilishi kutoka Benki ya
Dunia (wa pili kushoto), Bi. Neema Ndunguru, Mkurugenzi wa Mazingira ya
Biashara (PDB) pamoja na wawakilishi kutoka Benki ya Dunia wakiwa meza kuu
wakati wa Kikao cha majadiliano katika ya Mahakama na Wadau wa Jumuiya ya
Wafanyabiashara kupata maoni juu ya maboresho ya huduma za Mahakama. (IMG.
7436)
Mmoja wa wadau walioshiriki katika warsha hiyo akitoa
maoni yake katika majadiliano hayo. (IMG. 7449)
Washiriki wakiwa katika kazi za makundi wakitoa maoni
juu ya Mpango Mkakati wa Mahakama wenye lengo la kuboresha utoaji wa huduma
zake. (IMG. 7465) (Picha na Mary Gwera,
Mahakama)
Na Mary Gwera
KATIKA mwendelezo wa maboresho ya utoaji wa huduma ya haki nchini,
Mahakama ya Tanzania inaendelea kufanya jitihada mbalimbali ikiwa ni pamoja na
kukutana na wadau pamoja na Washirika mbalimbali wa maendeleo ili kupata maoni
yao juu ya uboreshaji wa huduma zake.
Akiongea na Waandishi wa Habari mapema jana, katika Warsha iliyoandaliwa
na Mahakama ikishirikisha Ugeni kutoka
Benki ya Dunia na Wawakilishi kutoka Jumuiya ya Wafanyabiashara kutoka, TRA,
Umoja wa Taasisi za Kifedha,MOAT, TIRA, TCRA n.k iliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli
ya Hyatt jijini Dar es Salaam, Bw. Hussein Kattanga, Mtendaji Mkuu wa Mahakama
ya Tanzania alisema Mahakama imekuwa katika mchakato wa maboresho na washirika
mbalimbali wa Maendeleo na wadau wa utoaji haki ili kuboresha huduma zake.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...