Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akibofya kitufye cha Lap Top kuashiria kufunga rasmi Matangazo ya Televisheni ya Analojia, baada ya kufikia ukomo rasmi hii leo Juni 17, 2015 baada ya kufanikiwa kuzima mitambo ya Analojia kwa nchi nzima. Sherehe hizo za ukomo zimefanyika leo kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Fenella Mukangara.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Tuzo ya Heshima za Digital Tanzania, Bi. Asteria Kamara, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, wakati wa sherehe za Ukomo wa Matangazo ya Televisheni ya Analojia, zilizofanyika leo Juni 17, 2015 kwenye ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof. Makame Mbarawa.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Tuzo ya Ngao ya Heshima za Digital Tanzania, Mkurugenzi Mkuu wa Mawasiliano Tanzania, TCRA, Prof, John Nkoma, wakati wa sherehe za Ukomo wa Matangazo ya Televisheni ya Analojia, zilizofanyika leo Juni 17, 2015 kwenye ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof. Makame Mbarawa. (wa pili kulia) ni Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo , Dkt. Fenella Mukangara. 

KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...