Mkurugenzi wa kampuni Exclusive media, Gody Gervas akizungumza na waandishi wa habari leo katika Hoteli ya Kebbys jijiji Dar es Salaam, Kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Qutub Global Ltd,Jeremia Fumbe na kulia ni  Mkurugenzi wa Kampuni ya Exclusive media (T)Ltd ESunday Mashele.

Na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.
KAMPUNI Exclusive media (T)Ltd ikishirikiana na Qutub Global Ltd kukutanisha Tasisi na Asasi za Kifedha hapa nchini  katika maonyesho ya Pesa Expo katika Maonyesho yatafanyika mwanzoni wa mwezi Septemba mwaka huu.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa kampuni Exclusive media, Gody Gervas wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Hoteli ya Kebbys jijiji Dar es Salaam leo.

 Gervas amesema Pesa Expo itahusiaha baadhi ya taasisi za kifedha ambazo zinaweza kushiriki katika maonyesho hayo ni pamoja na Mabenki, Saccos,Makampuni ya Bima, Makampuni yanayotoa huduma za mikopo,makampuni yanayotoa huduma za fedha za kieletroniki, Mifuko ya hifadhi ya jamii, Makampuni yanayotoa huduma za kutuma fedha,Soko la hisa na madalali wake,Makampuni yanayotoa huduma za ushauri wa kifedha na Taasisi zisizo na faida zinazotoa elimu kuhusu mambo ya fedha.

Gervas ameongeza kuwa  makampuni ambayo hayaja thibitisha ushiriki katik maonyesho hayo wadhibitishe ili kuwapa elimu wananchi  kuhusiana na huduma nyingi za kifedha zinazotolewa hapa nchini.

Amesongeza kuwa  makampuni yatakayoshiriki katika maonyesho hayo ni kufanya mauzo ya moja kwa moja, kutangaza huduma zao mpya, kutoa elimu ya huduma kwa wananchi, kuboresha mahusiano baina ya makampuni shiriki,kubadilishana mawazo na wajasiliamali na 
wananchi,kufanya tafiti ya bidhaa zao pamoja na kujitangaza.

Maonyesho hayo ya  Pesa Expo yataanzia jijini Dar es Salaam na baadae  mikoa mingine.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...