Mgeni rasmi katika mchezo wa robo fainali ya Netiboli kati ya Mtwara dhidi ya Mwanza Bibi Odilio Mushi ambaye pia ni Afisa Elimu Mkuu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI akitoa nasaha kwa wanamichezo hao mara baada ya kuzikagua timu zao  katika viwanja vya Chuo cha Ualimu cha Butimba, Mwanza.
 Waamuzi wa mchezo wa riadha wanaoshiriki katika mashindano ya UMITASHUMTA wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufanyika kwa fainali ya mbio za mita 400 yanayoendelea katika viwanja vya Chuo cha Ualimu cha Butimba, Mwanza.
-------------------------------------------------
Matokeo ya mpira wa miguu kwa wavulana yanaonyesha kuwa Ruvuma na Katavi  zilitoka sare ya 1-1, Tanga walifungwa na Rukwa  2-1, huku Kilimanjaro ilitoka sare ya 1-1 na Tabora. Pia Shinyanga iliifunga pwani 1-0, Kigoma iliifunga Iringa mabao 2-0 huku Mbeya ikaibamiza Manyara 4-0.
Matokeo ya mpira wa wavu kwa wavulana yanaonyesha kuwaMtwara ilishinda Mara kwa seti 2-0, Mwanza ikaichapa Shinyanga seti 2-0, Manyara ikaishinda Tabora seti 2-0, na Ruvuma ikaichabanga Kilimanjaro seti 2-0.
Kwa upande wa wasichana Tanga ikaifunga Shinyanga seti 2-0, Mtwara iliichabanga Manyara seti 2-0, Kigoma iliifunga Singida seti 2-0 na Katavi iliilaza Simiyu seti 2-0.
Katika mpira wa mikono kwa wavulana Rukwa iliichapa Manyara mabao 15-10, Dar es salaam iliichapa na Tabora mabao 31-11, Singida ilifungwa na Mwanza mabao 20-5, ma Morogoro iliifunga Kigoma  mabao 15-8.
Katika mchezo wa mpira wa mikono wasichana, Geita iliichapa Tabora mabao 24-6, Pwani iliifunga Iringa mabao 7-5, huku timu za Mbeya na Lindi zilitoka sare mabao 11-11m na Tanga iliichabanga Manyara mabao 11-2.
Kwa upande wa mpira wa Netiboli, Arusha iliifungaSimiyu mabao 29-13,  Katavi ilifungwa na Morogoro mabao 36-18, Mbeya iliichakaza Manyara mabao 31-16, Dodoma iliifunga Singida mabao 21-12 na Lindi iliilaza Kigoma mabao 38-36.
Matokeo ya mpira wa kengele kwa wavulana yanaonyesha Mtwara iliifunga Mbeya mabao 11-3, Kilimanjaro iliifunga Singida mabao 8-5, Dodoma ilifungwa na Kagera mabao 9-11 na Manyara iliifunga Tabora mabao 5-2.

Kwa upande wa mpira wa kengele wasichana Kilimanjaro iliifunga Singida mabao 10-3 na Kagera iliilaza Tabora mabao 9-4.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...