Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza Stanslaus Mabula (pichani) kesho Jumamosi atafunga rasmi mashindano ya Taifa ya Vijana wenye umri chini ya miaka 13.
Sherehe ya kufunga mashindano hayo itafanyika katika uwanja wa CCM Kirumba kuanzia majira ya saa9 kamili alasiri .
Kwa takribani wiki moja sasa mashindano hayo yamekuea yakiendelea jijini Mwanza katika viwanja vya Alliance na CCM Kirumba.
Lengo la mashindano haya ni kuibua vipaji kwa ajili ya kupata timu ya Taifa ya awali itakayojiandaa na fainali za vijana Afrika wenye umri chini ya miaka 17 mwaka 2019 fainali zitafakazonyika nchini Tanzania.
Katika kutambua na kujiunga na watanzania wenzetu wenye ulemavu wa ngozi (Albino) siku hiyo ya tareje 13/06/2015, TFF itajiunga na familia ya walemavu wa ngozi katika kuadhimisha siku yao kimataifa na kuonyesha bango maalum leney kuelimisha umma juu ya ubaya wa uovu wa kuwaumiza na kuwaua wenzetu wenye ulemavu wa ngozi.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO
LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...