Maandalizi ya kutandaza mkeka wa uhakika katika Barabara ya kutokea Hedaru mpaka Same mkoani Kilimanjaro umekuwa ukienda vyema kadri siku zinavyokwenda na kuleta matumaini ya safari njema na ya uhakika kwa watumiani wa barabara hiyo, pichani ni moja ya gari likipita kwenye barabara ya muda wakati mkema wa ukweli ukiendelea kutandandazwa.
 Mafundi wa Ujenzi wa barabara hiyo wakiendela na kazi, ili kuhakikisha mkeka wa uhakika unapatikana haraka iwezekanavyo.
 Sehemu ya mchekupuko.
 Muonekano wa barabara ya zamani huku ya muda ikiendelea kuandaliwa.
Ili kupatikana mkeka ulio bora, ni lazima umwagiliaji uhusike.
Mmoja wa wataalam wa Ujenzi wa barabara hiyo akipitia nyuzzzzz....

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 12, 2015

    Kazi kubwa imefanyika ya ujenzi wa barabara tuendelee na kazi nzuri hii.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 12, 2015

    Nilipita barabara ya Bukoba Karagwe ilipokuwa ni mbaya sana miaka ya nyuma wakati huu lori za kahawa tu ndiyo zilikuwa zinatumika zaidi,kufika ilikuwa inatumia muda mrefu, nikapita wakati msamaha wa madeni umeiwezesha barabara hii kupitika kwa wakati wote ikawa afadhali. Baadaye lami ikawa mpaka Kyaka, sasa lami mpaka Bugene, safari imekuwa fupi, maendeleo yapo.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 12, 2015

    CCM yajenga Nchi

    Tango Mike - Arusha

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 12, 2015

    Nadhani katika eneo ambalo utawala huu unaweza kujivunia pasipo shaka ni ujenzi wa miundo mbinu ya barabara. .

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...