MHARIRI Msanifu wa Gazeti la Mtanzania, Khamis Mkotya (35) juzi alitangaza rasmi nia ya kugombea ubunge katika Jimbo la Chemba, lililopo Mkoa wa Dodoma.
Mkotya ambaye kitaaluma ni mwandishi wa habari na kijana msomi mwenye Shahada ya Siasa na Uongozi, alitangaza nia hiyo mbele ya waandishi wa habari, katika ukumbi wa Dodoma Hotel.
Mkotya ambaye ni kada wa Chama Cha Mapinduzi ni miongoni mwa waandishi wa habari za Bunge, ambaye amekuwa mstari wa mbele katika kuwatetea wananchi wa Chemba kupitia taaluma yake.
Akizungumza katika mkutano huo, Mkotya ambaye ni mzaliwa wa Kijiji cha Mirijo Chini wilayani Chemba, alisema changamoto za jimbo hilo ndizo zilizomsukuma kuwania nafasi hiyo.
Katika mkutano huo, Mkotya alisema kwa muda mrefu ametumia taaluma yake kupiga kelele kuibua matatizo na kero za wananchi wa Chemba na baadhi kupatiwa ufumbuzi, hivyo umefika muda kuomba ridhaa yao ili aweze kuwatumikia kimamlaka zaidi.
Uzoefu wake katika masuala ya Bunge kama mwandishi wa habari za Bunge, pia utakuwa chachu na msaada mkubwa kwake katika kutimiza dhana ya uwakilishi ndani ya Bunge.
Ndugu zangu sijakurupuka katika kufikia uamuzi huu, nimekaa, nimetafakari na kujipima mwenyewe na kubaini kwamba ninatosha. Uwezo wa kutekeleza majukumu ya kibunge ninao, nia ya kuwatumikia wananchi wa Chemba ninayo na sababu za kugombea ninazo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...