Mhariri  wa Mwana Halisi Online, Edson Kamukara (pichani), amefariki Dunia kwa ajali ya moto nyumbani kwake Mabibo jijini Dar es Salaam leo hii majira ya saa moja kasorobo jioni, baada ya kulipukiwa na jiko la gesi, habari zilizotufikia sasa hivi zinasema kuwa Polisi wameuchukua mwili wa marehemu na kwenda kuhifadhi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya uchunguzi wa kifo chake.

Ofisa Uhusiano wa NMB, Viccent Mnyanyika akimkabidhi zawadi marehemu Edson Kamukara wakati wa uhai wake kwenye wa utoaji wa tuzo za Umahiri za Uandishi wa Habari Tanzania (EJAT) zilizofanyika Aprili 24 mwaka huu.
Globu ya Jamii inaungana na familia ya marehemu, ndugu, jamaa, wafanyakazi wenzake, marafiki na majirani katika msiba huu. Mola na aiweke mahala pema Roho ya Marehemu,
AMINA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 26, 2015

    Poleni sana wafiwa, so young and gone too soon!!

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 26, 2015

    Je tunatakiwa kuboresha usalama na viwango vya majiko au mitungi ya gesi inayotumika, tukio hili lakusikitisha litusukume pia kuangalia swala hilo pia, au ilikuwa tu ajali?.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...