Zimekusanywa na 
Samuel Kamugisha


CHANNEL 10
*Baraza la Taifa la elimu ya ufundi NACTE lafuta usajili wa vyuo 3 na 16 kushushwa hadhi katika jitihada za kulinda ubora wa elimu nchini. http://youtu.be/2HosRmHz7lU

*Jaji Augustino Ramadhani apata wadhamini mkoani Kilimanjaro huku akisema endapo atachaguliwa atashirikiana na wagombea wenziwe. http://youtu.be/qU7V9hQfIlI
 *Kada wa CCM Edward Lowassa asema hababaishwi na kashfa,vitisho na matusi anavyokumbana navyo kwani ana nia ya dhati ya kuongoza taifa. http://youtu.be/E3B2b4y_uiQ 
 *Chama cha Mapinduzi Zanzibar kimesema kitendo cha wajumbe na mawaziri wa CUF kususia kikao cha Bajeti ni kinyume cha Katiba. http://youtu.be/2UiljpCNCho    
 *Jaji mkuu Othman Chande azindua majarida ya sheria yanayo husu maamuzi ama hukumu za mahakama kuu ikiwa ni mara ya kwanza nchini. http://youtu.be/pvJ_xL6GZD4
 *Kituo cha sheria na haki za binadamu kimezindua taarifa ya haki za binadamu na biashara 2014 huku ikionyesha ukiukwaji mkubwa wa haki. http://youtu.be/VtNbOW6H3tM  
 *Wananchi wilayani Misungwi waiomba serikali msaada wa chakula kufuatia njaa katika wilaya hiyo baada ya mvua kusomba chakula chao. http://youtu.be/gYD1YcRD6uA 
 STAR TV NEWS
*Raisi Kikwete ataka Tanzania kutondokana na utegemezi huku akitaka raisi ajaye kuwekeza mageuzi makubwa ya sayansi na teknolojia.  http://youtu.be/zRVrFA5SunQ 
 *Dr. Mwele Malecela awataka wanawake nchini kutumia fursa ya uchaguzi mkuu ujao kuhakikisha wanawania uongozi ili kuwa miongoni mwa vyombo vya maamuzi nchini. http://youtu.be/XJBQMYwTJRM  
 *Ajali ya moto yatokea katika msikiti wa Masjid Omar jijini Dar es salaam huku sheikh wa msikiti huo akiwataka waumini wake kuwa watulivu. http://youtu.be/qlm9AeNgQGA 
 *Njia mpya ya utalii yabuniwa nchini itakayo wafanya watembelee vituo mbalimbali ya asili nchini.http://youtu.be/m41j6KgBbmU    
 AZAM TV NEWS
 *Madaktari wasema mavazi aina ya skin Jeans yanaharibu misuli na mishipa ya damu hivyo kuleta madhara kiafya.http://youtu.be/72C-dyJvjLI   
 *Vijana washauriwa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha BVR ili kupata fursa ya kuchagua viongozi wanao wahitaji .http://youtu.be/bHPSBbD9ozU  
*Wazee wasiojiweza na walemavu mkoani Mwanza wanakabiliwa na hali ngumu ya kimaisha baada ya Mzabuni kusitisha utoaji huduma kwa wazee hao kwa kinachodaiwa kuwa deni kubwa. http://youtu.be/12_tDsCctXw     
TBC NEWS
*Watu 6 wakiwemo raia 3 wa Kenya watiwa mbaroni mkoani Mara kwa kosa la kujaribu kuvuruga zoezi la uandikishaji wapiga kura BVR. http://youtu.be/uGcO0gnyNVo       
*Jeshi la polisi Mkoani Manyara linawashikilia watu 3 kwa tuhuma za kujiandikisha mara mbili katika daftari la wapiga kura.http://youtu.be/G9BOu7RITL0
 *Chama cha Mapinduzi kimeishauri serikali kurejesha mswada wa habari kwa wadau wa habari kabla ya kuupeleka bungeni ili kuweze kupatika muafaka. http://youtu.be/PGkhpqD-dxg   
 *Kamati kuu ya CCM inatarajiwa kukutana mwishoni mwa wiki hii mjini Dodoma chini ya mwenyekiti wake Dr.Jakaya Mrisho Kikwete. http://youtu.be/Skg38Hrx0r4   

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 25, 2015

    This is a good move...inatuwezesha tulio nje ya nchi kupata summary ya news za nyumbani Tanzania. Big up Simu TV

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...