MWANDISHI wa habari mwandamizi wa Shirika la Utangazaji nchini TBC FLORENCY DYAULI (Pichani enzi za uhai wake)amefariki dunia usiku wa kuamkia leo baada ya kuugua.

FRORENCE DYAULI amefariki dunia majira ya saa kumi alfajiri akiwa amelazwa katika hospitali ya RABININSIA MEMORIAL jijini  Dar es Salaam, ambako alikuwa akipata matibabu.

Dyauli alizaliwa  tarehe   27 mwezi wa saba mwaka 1961 na amefariki dunia tarehe   18/06/2015.
Marehemu DYAULI alisoma shule ya msingi   CHANG’OMBE mwaka 1968 hadi 1975.
Alipata elimu ya sekondari mwa 1976 hadi 1979 katika shule ya wasichana KISUTU jijijini Dar es Salaam.
Baadae alijiunga na Chuo cha Uhazili TABORA na kupata cheti katika fani ya katibu muhtasi mwaka 1980 hadi 1981.
Marehemu DYAULI alipata stashahada ya uandishi wa habari  mwaka 1988 katika chuo cha Uandishi wa habari TSJ jijini Dar es Salaam.
Taratibu za mipango ya mazishi tutaendelea kuwajulisha katika taarifa zetu zijazo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 18, 2015

    Poleni sana kwa msiba mkubwa uliyowapata Mungu amlaze mahali pepa poponi. Amina

    mary kahabuka

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...