Benki ya NMB imedhamini mkutano mkuu wa Mwaka wa Makanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Tanzania bara ulioanza leo mkoani Mororogoro. 

Katika mkutano huo, NMB imeweka mabanda ya maonyesho yanayotoa elimu juu ya huduma mbalimbali zinazopatikana ndani ya benki ya NMB pamoja na kutoa huduma za papo kwa papo ambapo wajumbe wa mkutano huo walipata wasaa wa kufungua akaunti za chap chap pamoja na kupata huduma za NMB Wakala. 

Kwa huduma za NMB Wakala, wateja wa NMB wanaweza kutoa na kuweka fedha kwenye akaunti zao za NMB bila ya kwenda kwenye tawi lolote la NMB.

Mkutano huo ulioanza leo, utafanyika kwa siku tano mpaka Ijumaa ya Tarehe 5, Juni, 2015.
Kamishna jenerali wa jeshi la Zimamoto na Uokoaji Tanzania bara - Pius Nyambacha akimsikiliza mfanyakazi wa benki ya NMB - Nehemiah Simba na akifafanua jambo wakati akieleza namna ya huduma ya kufungua akaunti ya NMB chapchap Instant account  mara baada ya ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka wa makanda wa jeshi la zimamoto na uokoaji Tanzania bara uliofanyika mkoani Morogoro leo.
 Meneja wa NMB kanda ya mashariki - Nazareth Lebbi akielezea jambo kwa Naibu Kamishna wa Utawala na Fedha jeshi la zimamoto na uokoaji - Billy Mwakatage na Mwakilishi wa mkuu wa wWilaya ya Morogoro - Ester Rugaira wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa makanda wa jeshi hilo mkoani Morogoro.
Meneja wa  NMB kanda ya mashariki - Nazareth Lebbi akizungumza jambo na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani -  Mwamini Malemi wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka wa makanda wa jeshi la zimamoto na uokoaji Tanzania bara uliofanyika mkoani Morogoro leo. katikati ni Kamishna jenerali wa jeshi hilo - Pius Nyambacha.
Kamishna Jenerali wa jeshi la zimamoto na uokoaji Tanzania bara - Pius Nyambacha akizungumza jambo na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa jeshi la Magereza - Dkt Kato Rugainunura wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa makanda wa jeshi hilo mkoani Morogoro. kulia ni Meneja wa NMB kanda ya mashariki - Nazareth Lebbi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...