Benki ya NMB imetoa msaada wa vifaa vya hospitali kwaajili ya zahanati ya chuo kikuu cha Dodoma vyenye thamani ya Shilingi milioni 20.
Vifaa hivyo vilivyotolewa kwa Makamu Mkuu wa Chuo kikuu cha Dodoma – Prof Shaaban Mlacha ni pamoja na - Jokofu kwaajili ya benki ya Damu, Meza ya upasuaji (Operating Table), Taa maalumu za kwenye chumba cha upasuaji (Overhead Operating Lamp) vyote vikiwa na thamani ya shilingi Milioni 20.
Msaada huo ulipokelewa vyema na uongozi wa chuo kikuu cha Dodoma kusifu juhudi za benki ya NMB katika kuchangia maendeleo nchini.
Afisa Mkuu wa Idara ya Wateja wa Jumla na Serikali wa NMB – Richard Makungwa akikabidhi taa maalumu za chumba cha upasuaji kwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma – Prof Shaaban Mlacha kwaajili ya zahanati ya chuo kikuu cha Dodoma. Pamoja na taa hizo, NMB pia ilikabidhi Jokofu la kutunzia damu ( Blood Bank), meza ya upasuaji ( Operating table) vyote vikiwa na thamani ya shilingi Milioni 20. NMB ilikabidhi vifaa hivyo ikiwa ni mchango wake kwa jumuia ya chuo kikuu cha Dodoma ili kuinua kiwango cha huduma zinazotolewa na zahanati hiyo.
Afisa Mkuu wa Idara ya Wateja wa Jumla na Serikali wa NMB – Richard Makungwa akikabidhi meza ya upasuaji (Operating table) kwa Makamu Mkuu wa Chuo hicho Prof Shaaban Mlacha kwaajili ya zahanati ya chuo kikuu cha Dodoma. Pamoja na taa hizo, NMB pia ilikabidhi Jokofu la kutunzia damu ( Blood Bank), meza ya upasuaji ( Operating table) vyote vikiwa na thamani ya shilingi Milioni 20. NMB ilikabidhi vifaa hivyo ikiwa ni mchango wake kwa jumuia ya chuo kikuu cha Dodoma ili kuinua kiwango cha huduma zinazotolewa katika zahanati hiyo.
Wafanyakazi wa NMB kanda ya Kati wakiwa katika picha ya pamoja mbele ya vifaa vya hospitali vilivyotolewa na NMB kwaajili ya zahanati ya chuo kikuu cha Dodoma. Katika kuhakikisha huduma za zahanati ya chuo kikuu cha Dodoma zinaboreshwa, NMB ilimkabidhi Makamu Mkuu wa Chuo cha Dodoma – Prof Shaban Mlancha taa maalumu za kufanyia upasuaji (overhead lamp) Jokofu la kutunzia damu ( Blood Bank), meza ya upasuaji ( Operating table) vyote vikiwa na thamani ya shilingi Milioni 20.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...