Meneja Mkuu wa Mauzo ,Wateja Wadogo na Wakubwa wa Benki ya DCB,Haika Machaku ,akizungumza na waandishi  wa habari juu ya uzinduzi wa filamu iitwayo Hamu ya Mafanikio itakayozinduliwa siku ya Jumamosi,25 June 2015 katika ukumbi wa Cinema wa Dar Free Zone.Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa CONSNET GROUP LTD,Sanctus Mtsimbe.
 Mkurugenzi Mtendaji wa CONSNET GROUP LTD,Sanctus Mtsimbe akizungumza na Waandishi wa Habari juu wa uzinduzi wa filamu hiyo siku ya Jumamosi,25 June 2015 katika ukumbi wa Cinema wa Dar Free Zone,kulia ni mwigizaji wa filamu hiyo,Mrisho Zimbwe(Tito)
Wawakilishi wa Benki ya DCB na Mwakilishi kutoka CONSNET GROUP LTD pamoja na Waandishi wa Habari wakisikiliza  maswali yaliyokuwa yanaulizwa yaliohusu uzinduzi wa filamu iitwayo Hamu ya Mafanikio itakayozinduliwa siku ya Jumamosi,25 June 2015 katika ukumbi wa Cinema wa Dar Free Zone.


Na Bakari Issa Madjeshi 
Rais Mstaafu,Benjamini Mkapa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa Filamu ya  Desire to Succeed ‘Hamu ya Mafanikio’uzinduzi wa filamu hiyo utaofanyika katika ukumbi  wa Cinema wa Dar Free Zone Juni  25 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Hayo yalisemwa na Meneja Mauzo,wateja wadogo na wakubwa wa Benki ya DCB,Haika Machaku wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake  jijini Dar es Salaam jana alisema kuwa  DCB wameamua kuandaa Filamu hiyo baada ya kutambua kuwa Watanzania wengi wanapenda kuangalia filamu za Kiswahili na hivyo wanaamini kuwa itaweza kuwafikia watu wengi na kufikisha ujumbe kirahisi zaidi.

Aidha  amesema katika filamu hiyo elimu,hamasa na faida mbalimbali za huduma za DCB Commercial Banki zimeonyeshwa.

Pia amesema  katika filamu hiyo imeeleza namna gani akaunti ya  Wanafunzi (DCB  Student Account) ilivyomsaidia kijana Jensen kupata elimu yake  hata baada ya kufiwa na wazazi wake.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Consnet Group,amesema lengo hasa la filamu hiyo ni kufikisha ujumbe kwa jamii lengwa ili kupata elimu ya kutosha juu ya huduma za Kibenki.

Filamu hiyo imeandaliwa Kampuni ya Consnet Group kwa kushirikiana na Benki ya  DCB  yenye lengo la kuelimisha na kuhamasisha wateja,wadau na umma kwa ujumla juu ya faida za kufanya shughuli za kibenki na DCB ambazo zinabadili maisha ya mhusika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...