Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Technolojia, Prof. Makame Mbarawa ameipongeza Kampuni ya HUAWEI Tanzania kwa ushirikiano wao wa karibu na wizara katika kuchangia miradi mingi hususan mambo mengi ya TEHAMA .

Huawei Tanzania inafanya kazi kwa ukaribu sana ni wizara na kwa hivi sasa ni mojawapo ya Mtoa huduma za vifaa vingi vya ujenzi wa jengo jipya la DATA center.

Data center ni mojawapo ya ujenzi mkubwa unaofanywa na wizara ya sayansi na jingo hili litakua na kazi ya kuhifadhi DATA za serikali pamoja na makampuni mbalimbali ya umma na ya binafsi. Data center itakuwa inahifadhi na kutunza kwa usalama takwimu na habari zozote kwa kutumia sever zake na kupelekea upatikanaji wa huduma kua kwa bei nafuu na kwa urahisi
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Patrick Makungu na Mkurugenzi Mtendaji wa Huawei Tanzania Zhang Yongquan wakitia saini Mkataba wa Makubaliano (MoU), kati ya Huawei Tanzania na Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia ambapo Huawei watakuwa washauri wakuu wa nchi katika maswala ya TEHAMA. Wakitizama (kutoka kulia hadi kushoto); Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa, Balozi wa China nchini Tanzania Balozi Lv Youqing na Naibu Waziri wa Afya wa Zanzibar Mahmoud Kombo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Huawei Tanzania Zhang Yongquan akitoa hotuba yake katika kongamano la Huawei Cloud Conference 2015, wakitazama (kutoka kushoto hadi kulia); Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa na Balozi wa China nchini Tanzania Balozi Lv Youqing.
Mkurugenzi Mtendaji wa Huawei Tanzania Zhang Yongquan na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa wakikata utepe kuzindua rasmi gari maalum la Huawei kwa ajili ya maonyesho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...