Mshiriki wa Mafunzo  ya  utekelezaji mradi wa Kuimarisha mfumo wa habari za hali ya hewa na mifumo ya tahadhari ya mapema nchini akichangia wakati wa mafunzo hayo kwa wajumbe wa kamati za maafa za kata ya Makiba, wilayani Arumeru mkoani Arusha, mafunzo hayo yameratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia mradi huo , Tarehe 13 Juni, 2015.
Mratibu mradi kitaifa wa Kuimarisha mfumo wa habari za hali ya hewa na mifumo ya tahadhari ya mapema nchini, Alfei Daniel akifafanua jambo wakati wa mafunzo ya utekelezaji wa mradi huo kwa wajumbe wa  kamati za maafa za kata ya Makiba, Wilayani Arumeru mkoani Arusha, tarehe 13 Juni, 2015, wengine ni wawezeshaji wa mafunzo hayo.

Washiriki kutoka kamati za maafa za kata ya Makiba, Wilayani  Arumeru mkoani Arusha, wakiwa katika picha ya pamoja na Mratibu mradi kitaifa wa Kuimarisha mfumo wa habari za hali ya hewa na mifumo ya tahadhari ya mapema nchini, Alfei Daniel (wa kwanza kushoto) mara baada ya kufunga mafunzo ya utekelezaji wa mradi huo, tarehe 13 Juni, 2015.

Serikali za vijiji zatakiwa kuhusisha Maafa ya mabadiliko ya tabianchi na mipango ya maendeleo. 
 Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Uratibu Maafa kupitia mradi wa kuimarisha mifumo ya habari za hali ya hewa na mifumo ya tahadhari nchini imezitaka serikali za mitaa na vijiji nchini kuhusisha maafa yatokanayo na mabadiliko ya tabianchi na mipango yao ya maendeleo, ili kuhakikisha jamii inakuwa na uchumi bora na uwezo wa kupunguza athari za maafa hayo. 

Akiongea wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wajumbe wa Kamati ya Maafa wa kata ya Makiba Wilayani Arumeru, mkoani Arusha, Mratibu Mradi huo Kitaifa, Alfei Daniel tarehe 13 Juni, 2015, alisema serikali za vijiji zitumie taarifa za athari za mabadiliko ya tabianchi za vijiji vyao ambazo zitakuwa zinaainishwa kupitia mradi huo kama sehemu ya kuandaa mipango mikakati ya maendeleo vijijini. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...