Waziri wa Nishati na Madini George Simbachawene (wa pili kushoto) akikagua miundombinu ya kuhifadhi mafuta katika Bohari ya Kampuni ya GBP ya Tanga.  Nyuma ya Waziri ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Said Magalula. Wengine kutoka kulia ni Meneja Mkuu wa PICL, Michael Mjinja, Kamishna wa Nishati na Maendeleo ya Petroli Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi, Hosea Mbise na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya GBP ya Tanga, Badar Masoud. Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa GBP, Bohari hiyo ina uwezo wa kuhifadhi lita milioni 26 za mafuta.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Bohari ya GBP ya Tanga, Badar Masoud akimwonesha akimweleza jambo Waziri wa Nishati na Madini George Simbachawene wakati akikagua miundombinu ya kuhifadhi mafuta katika Bohari ya Kampuni ya  GBP , Tanga. Wengine katika picha ni Baadhi ya watendaji wa Wizara  na wadau wa mafuta mKoa wa Tanga zikiwemo Taasisi za Serikali.
 Mhandisi katika Kampuni ya TSN Group, ambao ni wamiliki wa  bohari ya kuhifadhi mafuta ya TAPCO Mhandisi Michael Shimiu,(wa tatu kulia) akimweleza jambo Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene (wa pili kushoto) na ujumbe wake wakati walipoitembelea Kampuni hiyo kuona miundombinu ya kuhifadhi mafuta ya Kampuni hiyo. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga Said Magalula na kulia ni Mkurugenzi wa TSN Group, Farouk Baghoza.
Kwa habari kamili na picha zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...