Waziri wa Nishati na Madini George Simbachawene (wa pili kushoto) akikagua
miundombinu ya kuhifadhi mafuta katika Bohari ya Kampuni ya GBP ya Tanga. Nyuma ya Waziri ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Said Magalula. Wengine kutoka
kulia ni Meneja Mkuu wa PICL, Michael Mjinja, Kamishna wa Nishati na Maendeleo
ya Petroli Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi, Hosea Mbise na Mkurugenzi
Mtendaji wa Kampuni ya GBP ya Tanga, Badar Masoud. Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa
GBP, Bohari hiyo ina uwezo wa kuhifadhi lita milioni 26 za mafuta.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bohari ya GBP ya Tanga, Badar Masoud
akimwonesha akimweleza jambo Waziri wa Nishati na Madini George Simbachawene
wakati akikagua miundombinu ya kuhifadhi mafuta katika Bohari ya Kampuni
ya GBP , Tanga. Wengine katika picha ni
Baadhi ya watendaji wa Wizara na wadau
wa mafuta mKoa wa Tanga zikiwemo Taasisi za Serikali.
Mhandisi katika Kampuni ya TSN Group, ambao ni wamiliki wa bohari ya kuhifadhi mafuta ya TAPCO Mhandisi
Michael Shimiu,(wa tatu kulia) akimweleza jambo Waziri wa Nishati na Madini,
George Simbachawene (wa pili kushoto) na ujumbe wake wakati walipoitembelea
Kampuni hiyo kuona miundombinu ya kuhifadhi mafuta ya Kampuni hiyo. Kushoto ni
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Said Magalula na kulia ni Mkurugenzi wa TSN Group, Farouk
Baghoza.
Kwa habari kamili na picha zaidi BOFYA HAPA
Kwa habari kamili na picha zaidi BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...