Waziri wa Nishati na Madini,  George Simbachawene, akizungumza na wananchi wa  Kijiji cha Mwilowe, Wilaya ya Mpwapwa, baada  kuzuia msafara wake   wakati  alipopita  katika Kijiji hicho wakati wa ziara ya kukagua Utekelezaji wa Mradi wa Umeme Vijijini Awamu ya Pili unaofadhiliwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Kutekelezwa na Shirika la Umeme Nchini, (TANESCO). Wanakijiji hao walimweleza Waziri kuwa kijiji chao pia kiunganishwe na umeme.
 Wananchi wa Kijiji cha Mwilowe wakizuia msafara wa Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene wakitaka kijiji hicho pia kiunganishwe na nishati hiyo. Waziri alikua katika ziara ya kutembelea na kukagua Utekelezaji wa Mradi wa Umeme Vijijini unaofadhiliwa na wakala wa Nishati Vijijini (REA) na kutekelezwa na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO).
 Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene akiangalia mfano wa mashine ya kusaga inayotumia umeme  wa mota aliyotengenezwa na Kijana katika Kijiji cha Lukole. Simbachawene aliahidi kumsaidia Kijana hiyo kuweza kufikia lengo lake.
  Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene akizindua Albam ya  nyimbo ya Kwaya ya Mtakatifu Agustino katika Kijiji cha  Kingiti, Kigango cha Kingiti, wilaya ya Mpwapwa wakati wa ziara yake ya kukagua Utekelezaji wa Mradi wa Umeme Vijijini, Awamu ya Pili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...