Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

SERIKALI imeandaa rasimu ya mkakati wa mawasiliano katika sekta ndogo ya mafuta na gesi ambayo itaweza kusaidia kutoa elimu kwa wananchi na kuwaondolea usumbufu w wa kupata taarifa potovu kuhusu kuwepo na gesi nchini.

Akizungumza  leo jijini Dar es Salaam leo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara  kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara,Fatma Dendegu,Alfred Luanda  amesema kumekuwa na uhaba wa elimu kwa wananchi juu ya masuala ya gesi na mafuta na kusababisha vurugu katika mkoa huo.

"Wananchi wamekuwa hawana elimu ya kutosha na kutokupewa ushirikishwaji kutoka serikalini katika masuala ya gesi hali ambayo inapelekea wananchi kuwa na imani potofu,"alisema.

Alisema mkakati huo wa elimu hiyo ya mawasiliano kwa wananchi utasaidia kwa kiasi kikubwa katika kuwahakikishia wananchi kuwa gesi iliyokuwqepo nchini ina faida kwa kila mwananchi.

Luanda alisema neema ya gesi iliyotokea nchini ni lazima ilindwe kwani  itasaidia katika kukuza uchumi wa nchi na kusaidia taifa kuwa katika uchumi wa kati kama inavyotegemewa katika miaka ijayo.

"Faida nyingine kubwa kwa kuwepo na gesi nchini  ni mchango mkubwa kuzalisha gesi hivyo itatumika kuzalisha umeme na taifa kuwa na umeme wa uhakika na wakutosha,"alisema.

Kwa upande wake,Meneja Mawasiliano wa Wizara ya Nishati na Madini Badra Masoud alisema mkakati huo unatarajia kukamilika mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu na baadae kuwapa wadau kuupitia na kwenda kwa wananchi.

"Mkakati huu utakuwa ni chachu ya kuwapa wananchi kuelewa rasilimali iliyokuwepo nchini na kuielewa faida yake na kuondokana na upotofu ambao wanaupata kutoka katika makundi mbalimbali,"alisema.

Alisema gesi ni raslimali ambayo ni kubwa nchini hivyo kuwepo nchini ina mchango mkubwa hivyo ni lazima wananchi wafaidike na kuitumia rasilimali hiyo kubwa. 
Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Fatma Salum Ally akizungumza na baadhi ya wananchi wa Wilya ya Lindi na Mtwara kuhusiana na matarajio makubwa katika sekta ya Mafuta na Gesi pamoja na uundwaji wa mikakati ya mawasiliano katika mkutano uliofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara Alfred Luanda  ambaye alikuwa mgeni rasmi akimwakilisha Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene akizungumza katika mkutano uliokutanisha baadhi ya wananchi wa Wilaya ya Lindi na Mtwara leo katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Msemaji wa wizara ya Nishati na Madaini akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na  Uwazi, Ushirikishwaji na uwajibikaji katika sekta ya mafuta na Gesi leo katika mkutano uliofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo. 

Baadhi ya wananchi wa wilaya ya Mtwara na Lindi waliohudhuria katika mkutano wa kujadiliana matarajio makubwa katika sekta ya mafuta na Gesi leo jijini Dar es Salaama katika hoteli ya Serena.(Picha na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...