Kamishna Msaidizi – Ukaguzi wa Migodi, Mhandisi Ally Samaje kutoka Wizara ya Nishati na Madini (Kushoto) akijadiliana jambo na Mtaalam mwelekezi kutoka Taasisi ya Sayansi na Mazingira ya Nchini India, Sujit Kumar Singh (Kulia) kwenye mafunzo yaliyoshirikisha wakaguzi wa migodini nchini yaliyofanyika mjini Bagamoyo mkoani Pwani.
Sehemu ya washiriki wa mafunzo yaliyoshirikisha wakaguzi wa migodini nchini yaliyofanyika mjini Bagamoyo mkoani Pwani wakishiriki katika zoezi la kuandaa mpango wa mazingira kwa vitendo katika mafunzo hayo.

Na Greyson Mwase, Bagamoyo

Taasisi ya Sayansi na Mazingira kutoka nchini India (Centre for Science and Environment) kwa kushirikiana na Wizara ya Nishati na Madini, imekamilisha mafunzo ya siku nne yaliyoshirikisha wakaguzi wa migodi nchini ambapo wakaguzi walijifunza jinsi ya kuandaa miongozo mbalimbali kwa ajili ya kutumika kwenye ukaguzi wa mazingira kwenye migodi.

Akizungumza katika mahojiano maalum wakati wa mafunzo hayo, Kamishna Msaidizi – Ukaguzi wa Migodi, Mhandisi Ally Samaje alisema lengo la mafunzo hayo lilikuwa ni kuwapa uelewa wakaguzi wa mazingira na migodi nchini wa kuandaa, kuchambua na kupitia taarifa za athari kwenye mazingira kutokana na shughuli za uchimbaji wa madini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...