Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager, leo imepoteza mchezo wake wa kwanza kuwania kufuzu kwa fainali za AFCON mwaka 2017 baada ya kufungwa kwa mabao 3 - 0 na wenyeji Misri.

Taifa Stars ilicheza vizuri kipindi cha kwanza na hasa sehemu ya ulinzi ilifanya kazi ya ziada kuokoa mashambulizi ya washambuliaji wa timu ya Misri, na kupelekea kwenda mapumziko -0 - 0.

Kipindi cha pili Misri walifanya mabadiliko yaliyowapelekea kupata mabao hayo 3 ndani ya dakika 10, kupitia kwa Ramy Rabia(60), Basem Morsy(64) na Mohamed Salah (69). 

Stars ilifanya mabadiliko ya kuwaingiza Frank Domayo, Saimon Msuva na Salim Mbdonde na kufanya shambulizi kadhaa langoni kwa Misri lakini mashambulzi hayo yaliokolewa na walinzi wa timu ya Misri.

Mara baada ya mchezo huo, Taifa Stars inaondoka leo Alexandria kuelekea Cairo ambapo itaondoka na shirika la ndege la Ethiopia saa 8 usiku na kufika jijini Dar es salaam jumanne saa 7 mchana.

Tanzania: Deogratias Munish, Shomari Kapombe, Oscar Joshua, Aggrey Morris/Salim Mbonde, Nadir Haroub, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Mwinyi Kazimoto/Saimon Msuva, Thomas Ulimwengu, Mbwana Samata, Amri Kiemba/Frank Domayo.

Misri: Ahmed El Shenawy, Ahmed Hegazy, Ramy Rabea, Mohamed Abd Elshafy, Hazem Emam, Mohamed Elneny, Ibrahim Salah, Mahmoud Abd Elmonem/Ramadan Soffiy, Mohamed Salah/Mostafa Ftahy, Doly Elgabay/Basem Morsy, Ahmed Hassan Meky.
USAJILI WA WACHEZAJI KUANZA JUNI 15

 Kikosi cha timu ya Taifa Taifa stars.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 15, 2015

    kWANI LAZIMA SISI TANZANIA KUSHIRIKI HAYA MASHINDANO AU KUCHEZA SOKA TUJARIBU BAO LABDA TUNAWEZA KUFIKA MBALI HII KUTUPA FEDHA NA KULITIA AIBU TAIFA LAZIMA TUCHOKE SASA IKO HAJA YA KUJITOA KATIKA MASHINDANO YA KIMATAIFA KWA MIAKA MITANO HUKU TUKITAFUTA VIPAJI KUANZIA MIAKA 17 VIJANA WAPYA WOTE SIO HII KAZI YA KU "RECYCLE" KILA MWAKA NA MATOKEO NI YALE YALE TUFIKIRI NJE YA SANDUKU AU ILE TAFSIRI YA MWENDA WAZIMU NDIO SISI,KUFANYA KITU KILE KILE NA KUTARAJIA MATOKEO TOFAUTI.

    MDAU.
    ALEXANDRIA,MISRI.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 15, 2015

    Niliangalia mechi hii.Taifa stars ni kichekesho ilicheza kibaya ni kama umewakusanya wachezaji kutoka mtaani masaa mawili kabla ya mechi. Hawana mpangilio na wangefungwa hata bao kumi kama WaMisri wangekuwa makini. Asilimia kubwa walikuwa wamisri waliotawala mechi. Hii ni aibu na Tanzania ifikirie kujitoa kwenye hii michezo na wajenge timu kwanza.
    Mdau Sweden.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...