Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Watanzania waishio Uholanzi waliojitokeza kumlaki wakati akiwasili jijini The Hague, Uholanzi, leo Jumatatu Juni 8, 2015.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo na muhtasari wa ziara yake toka kwa Balozi wa Tanzania nchini Uholani Mhe Wilson Masilingi baada ya kuwasili The Hague leo Jumatatu Juni 8, 2015.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Rais wa Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai ICC Jaji Silvia Alejandra Fernandes de Gurmendi alipotembelea makao makuu ya mahakama hiyo jijini The Hague leo Jumatatu Juni 8, 2015.
Rais Jakaya Kikwete akiongea na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uholanzi Mhe. Bert Koenders jijini The Hague leo Jumatatu Juni 8, 2015.



Watanzania wanaoishi nje ya Nchi wangependa serikali ijayo iendeleze na kudumisha juhudi za kuimarisha uchumi kuanzia pale ambapo Rais Jakaya Mrisho Kikwete ameishia katika utawala wake.

Jumuiya ya Watanzanzia wanaoishi nchini Uholanzi (TANE) wamemueleza Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika risala yao iliyosomwa na Makamu Mwenyekiti wa Mpito Bwana Johannes Rwanzo, ambapo Rais amepata fursa ya kuzungumza na Watanzania hao jioni ya tarehe 8 Juni2015, katika Hoteli ya Crowne Plaza, mjini The Hague .

"Tunaomba serikali ijayo iendeleze pale utakapoishia". Amesema Bw. Rwanzo. “Tunajua kuna mambo mengi ambayo labda muda wa awamu mbili hautoshi kuyakamilisha, basi tungeomba mambo haya uweze kuyakabidhi kwenye utawala unaofuata ili waendeleze pale utakapokuwa umefikia" ameongeza.

Bw. Rwanzo ameyataja baadhi ya mambo ambayo yanahitajika kuendelezwa na awamu ijayo kuwa ni pamoja na juhudi za kupambana na umaskini nchini na  ujenzi wa miundombinu.

Watanzania hao pia wamemuomba Rais Kikwete kuwa, pamoja na kustaafu, bado wangependa aendelee kutoa msaada kwa wananchi wa Tanzania kwani "Kustaafu sio mwisho wa kusaidia jamii".

Tangu kuingia madarakani, Rais Kikwete amekuwa na utaratibu wa kukutana na Watanzania wanaoishi nje ya Nchi kila anapofanya ziara katika Nchi mbalimbali na kuwaeleza maendeleo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Watanzania hao nao wamekuwa na jadi ya kumsomea risala, kumuuliza maswali kwa nia ya kupata  ufafanuzi wa masuala muhimu na kumpa Zawadi za aina mbalimbali.

Rais Kikwete yuko katika ziara ya kikazi  ya  kuishukuru Nchi ya Uholanzi kwa misaada ya kimaendeleo na pia kuiomba iendelee kuisaidia Tanzania ili iweze kukamilisha na kuendeleza juhudi za kujenga na kuimarisha uchumi kwa nia ya kuleta maendeleo Tanzania.

Rais Kikwete amepata fursa ya kuwaeleza Watanzania kuhusu uchaguzi Mkuu ujao ambao ameahidi kuwa utasimamiwa vizuri ili Watanzania wapate nafasi ya kuchagua viongozi wanaowataka.

Rais pia  amewaeleza Watanzania kuhusu juhudi mbalimbali za maendeleo ambazo amezifanya katika kipindi cha utawala wake  ambazo zimechangia kukua kwa uchumi na Nchi kujijengea  uwezo na  kujiletea maendeleo.

Rais ametumia fursa hiyo kuelezea jitihada zilizofanyika katika ujenzi wa barabara,  elimu, afya,  maji  na maendeleo katika teknolojia. Rais Kikwete amemaliza ziara yake katika Nchi za Finland, Sweden na Uholanzi na anatarajia kuondoka Uholanzi tarehe  9 Juni,2015 asubuhi na kuwasili Dar es Salaam jioni.

Imetolewa na;
Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,
The Haque – Uholanzi.
9 Juni, 2015

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 09, 2015

    Mheshimiwa Mkuu Rais JK umetika chicha sana baba hiko kiatu mzee naomba siku moja ufanye kama umevisahau nje msikitini wasela wako tujiokotee

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...