Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe leo June 8, 2015 amechukua fomu za kuomba ridhaa ya kugombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) makao makuu ya chama hicho mjini Dodoma baada ya kutangaza nia hiyo jana (Jumapili).
Waziri Membe akipokelewa fomu na Mkewe Dorcas mara baada ya kukabidhiwa fomu mjini Dodoma.
alipokelewa na makada na wafuasi wa chama hicho mjini Dodoma baada ya kukabidhiwa fomu hiyo na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa Oganaizesheni, Seif Khatib ambapo baada ya kupokea fomu hiyo Membe alisema; “Ninafurahi kukabidhiwa fomu hii na nina hakika kutokana na kujipima na kujiona ninafiti nafasi hii kulinganisha na waombaji wengine ni lazima tubadilishe nchi yetu kuwa nchi ya uchumi wa viwanda.”
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...