Picha na maktaba
Na Woinde Shizza,Arusha 
Mamlaka ya Chakula na dawa(TFDA) na Shirika la Viwango nchini(TBS), wameshauriwa kuwadhibiti zaidi wafanyabiashara wasio waaminini ambao wanaingia nchini bidhaa sizizo na ubora kwani wanaporomosha uchumi.

Meneja masoko wa kampuni ya  Wrigleys (EA) Company Ltd, Emanuel Laswai, alitoa kauli hiyo juzi, katika uzinduzi wa bidhaa mpya za kampuni hiyo ya Doublemint  nchini Tanzania.

Laswai alisema, uingizwaji wa bidhaa feki na zisizo na ubora zina  athari za kiuchumi na kiafya kwa watumiaji wa bidhaa hizo.

“sisi kampuni yetu kwa mwaka tunalipa kodi Tsh 120 milioni, lakini inaumiza kuona kuna bidhaa zinaingizwa nchini kinyamela bila kulipiwa kodi”alisema

Alisema bidhaa zao zote kabla ya kuingia sokono lazima ziidhinishwe na vyombo vya ukaguzi wa serikali kama TBS na TFDA.

Mkaguzi wa vyakula, dawa, vipodozi ,wa mamlaka ya chakula na dawa TFDA,kanda ya kaskazini, Barnabas Jacob, akizungumzia tatizo la uingizwaji bidhaa feki alisema Mamlaka hiyo, imeendelea kudhibiti na kukamata na kutekeleza bidhaa hizo.

Jakob alisema   milango ya TFDA, iko wazi kwa kila mwananchi kutoa taarifa ya kuwepo kwa bidhaa hatarishi katika mazingira yeyote ili ziweze kuchukuliwa hatua za kudhibiti  bidhaa zisizofaa kwa matumizi ya binadamu.

Kwa Upande wake, Afisa uhusiano wa  shirika la viwango nchini(TBS) Roida Andusamile akizungumza na Mwananchi alisema TBS itaendelea kudhibiti bidhaa zisizo na ubora kuingia nchini   kwa kuanza kudhibiti bidhaa hizo kutoka nchi zinapotoka.

Hata hivyo, alisema ni wajibu wa wananchi pia kutoa taarifa TBS wanapobaini bidhaa zisizo na ubora katika soko au ambazo bado hazijaidhinishwa na vyombo vya serikali, ili kuweza kuchukuliwa hatua mara moja ya kuwadhibiti na kuwakamata wahusika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...