Na Chalila Kibuda ,Globu ya Jamii, Tabora.

Waziri wa Uchukuzi,Samwel Sitta amesema kuwa anataka Urais wa miaka mitano kuweza kuivusha nchi katika kutokana na mambo yanayoonekana ikiwamo muungano,udini ,ungezeko la vijana.

Sitta ameyasema hayo leo wakati akitangaza nia ya kugombea urais katika mkutano uliofanyika katika viwanja  vya Ikulu ya Chifu Fundikira Kata ya Itetemia  mkoani Tabora.

Amesema mtu  yeyote makini ana nafasi ya Urais, hana budi   kuyapima mazingira ya taifa katika miaka mitano ijayo na kuzielewa changamoto zitakazokuwepo katika kipindi cha uongozi anachokusudia kuongoza.

“Maoni yangu kipindi cha miaka mitano ijayo kina mwelekeo wa mifarakano katika  masuala ya muungano wetu; kutetereka  kwa mshikamano wetu kunatokana na chokochoko  za siasa za ushindani, udini  na  kupanuka kwa  tofauti ya kipato, ongezeko la kundi kubwa  hususani la vijana mijini  lisilo  na uhakika wa ajira na haya yote yanaashiria ongezeko la uhalifu”amesema Sitta.

Amesema anamini kutokana na  mchanganyiko wa uzoefu  wa uongozi, unamuwezesha kukusanya  nguvu chanya za Watanzania ili kuyatanzua matatizo yanayotokana na changamoto zilizopo kwa kipindi cha sasa.

Sitta amesEma kugombea nafasi ya Urais wa nchi yetu si jambo jepesi.Linahitaji tafakuri ya kina ukizingatia kuwa nafasi hiyo ya uongozi inabeba matumaini ya watanzania wote milioni 47.

Amesema Ili kukuza uchumi wa nchi kwa kasi  inayopunguza umaskini kwa haraka na  huku  tukijenga uwezo mkubwa zaidi wa bajeti ya serikali kutosheleza ubora wa  huduma za jamii kama vile afya, elimu na maji, hatuna budi kufanya jitihada za makusudi za kuubadili mfumo wa uendeshaji nchi uwe ni wa motisha kwa wazalishamali. 

Mifumo ya nchi zilizopiga hatua kubwa za maendeleo duniani ni ile iliyoweka mazingira chanya ya kuaminiana baina ya serikali na sekta binafsi. Hali hii  haijatimia  hapa kwetu.

Aidha Wafanyabiashara wakubwa wa ndani hawawekezi vya kutosha ndani ya nchi kuleta maendeleo ya haraka ya huduma, viwanda,kilimo na biashara. Baadhi yao, kwa hakika baada ya kuchuma fedha wanazihamishia nje ya nchi. Matokeo yake ni kwamba uchumi haukui kufikia kiwango cha kutosheleza vipato vya wakulima na wafanyakazi na wafanya biashara.Hatuna budi kujenga muafaka na wafanyabiashara hususani wazawa wa nchi yetu. Kazi hii ina hatua mbili:

Amesema wafanyabiashara watachukuliwa hatua kwa wasio waaminifu kwa kukwepa kodi, wanaotorosha fedha za kigeni na wanaoshiriki katika rushwa kubwa na biashara za magendo,kuwepo kwa mshikamano baina ya wafanyabiashara waovu na watendaji serikali kunachochea rushwa na kudumaza uchumi. Hali hii lazima irekebishwe.
 Mheshimiwa Sitta akisimikwa kuwa Mjukuu Mkuu wa ukoo wa Fundikira katika hafla iliyofanyika katika viwanja vya Ikulu ya Unyanyembe Itetemia mkoani Tabora jana.
 Mheshimiwa Samweli Sitta akiwa na viongozi wenzake wa CCM alipokuwa akitangaza nia ya Kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 Mheshimiwa Samweli Sitta akitangaza nia mbele ya umati wa wananchi katika uwanja wa Ikulu ya Unyanyembe katika manispaa ya Tabora.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 03, 2015

    Miaka 5 - Uliza Nkurunzinza. Wenzio walikwishastaafu zamani sana wewe bado upoupo tu. Sasa unasema miaka 5 tu. Si uongo tu huo?

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 04, 2015

    Miaka mitano wewe sasa upate...wewe ni kiongozi hodari, unaheshimiwa, umefanya kazi safi miaka mingi, bila corruption yoyote. Kura yangu ishapata....

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...