Katika kuonyesha kuwa Benki ya Posta Tanzania (TPB), inafanya inatoa huduma za kibenki, lakini pia iko mstari wa mbele kuwajali wateja wake na wananchi kwa ujumla. Katika kutekeleza hilo,  wafanyakazi wa benki hiyo, wakiongozwa na Mkurugenzi Mkuu, Sabasaba Moshingi, wamejitolea damu, "kutunisha" benki ya taifa ya damu na hivyo kuokoa maisha ya watanzania ambapo miongoni mwao ni wateja wake. Zoezi la kutoa damu lilifanyika makao makuu ya benki hiyo barabara ya Samora jijini Dar es Salaam. Pichani Mkurugenzi Mkuu wa benki hiyo, Sabasaba Moshingi, akiwaongoza wafanyakazi wake, katika zoezi hilo.
 Mtaalamu wa masuala ya damu, (kushoto), akimpatia maelezo Meneja Mkuu anayeshughulikia masuala ya kampuni, Norvis Moes, kuhusu utoaji damu
 Moshingi, (kushoto), na mmoja wa wafanyakazi wa TPB, wakitolewa damu kwenye zoezi hilo.

PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...