
Maafisa
wa serikali ya Tunisia wamesema kuwa mmoja wa washambuliaji hao aliuawa kwa
kupigwa risasi na maafisa wa ulinzi na kuwa waliosalia bado wanasakwa na
polisi.
Shambulio
hilo lilitokea katika mji wa Sousse, ambao huwavutia maelfu ya watalii kutoka
bara Ulaya na Afrika ya Kaskazini.
Hili
lilikuwa shambulizi la pili dhidi ya hoteli ya watalii nchini Tunisia katika
kipindi cha miezi michache iliyopita.
Inaaminika
kuwa washambuliaji hao waliwavamia watalii ufukweni.
Mnamo
mwezi Machi mwaka huu, wanamgambo wa Kiislamu waliokuwa wamejihami kwa bunduki
waliwauawa zaidi ya watu 26 katika makavazi ya Bardo, iliyoko katika mji mkuu
wa nchi hiyo Tunis.Makavazi hayo ya Bardo hilo lilikuwa maarufu sana kwa
watalii.
October
mwaka wa 2013, mlipuaji wa kujitoa, alijilipua nje ya nyumba moja mjini Sousse,
baada ya maafisa wa polisi kutibua jaribio lake la kutaka kuingia ndani na
kuishambulia.
Chanzo BBC Swahili.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...