Hivi ndivyo hali ilivyo katika barabara hii ya Viwandani, Chang'ombe jijini Dar es salaam. uharibufu huu wa barabara umetokana na Mvua kubwa zilizokuwa zikinyesha maeneo mengi hapa nchi majuma kadhaa yaliyopita. Cha ajabu katika eneo hili bado maji ni mengi sana yametuama na huku uharibifu mkubwa wa barabara ukiendelea. Mzee wa Mtaa kwa Mtaa alibahatika kuzungumza na wadau kadhaa waliopo jirani na eneo hilo, ambapo walisema kuwa kuja kwa Dimbwi hilo ni kutokana na kutokuwepo kwa sehemu ya kusafirishia maji hayo kutokana na ujenzi holela wa Maghala na Viwanda vilivyolizunguka eneo hilo, hali inayopelekea kuwepo kwa adha hiyo kwa sasa. Je ni kweli kwamba ujenzi holela katika maeneo haya unapelekea kujaa kwa maji haya barabara??? Wataalam wa barabara tunaomba majibu. Picha zote na Othman Michuzi.
 Ile kauli ya "Kufa kufaana" ndiyo inayotumiaka hivi sasa katika eneo hili, kwani kuna baadhi ya vijana ambao wanaombea maji haya yaendelee kuwepo ili na wao wajipatie chochote kitu ili siku zisonge mbele. Pichani ni mmoja wa vijana hao akiiongoza moja ya gari kupita katika eneo salama bila kukwama, ambapo ujira wake ni kuanzia shilingi Elfu moja na kuendelea kutegemena na ubinaadamu wako.
 Kazi ikiendelea ya kuyapitisha magari katika maeneo salama.

BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 10, 2015

    Du umasikini usieolezeka. Kwa shilingi elfu moja anachukua risk na kupita kwenye hayo maji machafu yaliyotuama na kuweza kuambukizwa magonjwa. Ndio maisha bora kwa kila Mtanzania. Rais Kikwete anakuja huku nchi za Scandinavia na kuwadanganya viongozi wa huku na baadhi ya WaTanzania kwamba maisha ni mazuri Tanzania na nhci imeendelea.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 11, 2015

    Mzee wa Mtaa kwa Mtaa upo sawa kabisa:Kujenga kwenye mikondo ya maji ndio tatizo kubwa na inasabisha hasara na upotevu mkubwa wa rasilimali kidogo tuliyonayo. Lakini tufanyeje wachache kati yetu wanatumia uwezo wa kipesa na kuleta hasara kama hizo na kubaki kupiga kelele na mayowe.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 11, 2015

    Wanaohusika warekebishe hali hii maji yapate njia na barabara iliyobomoka ijengwe ili isiharibike kabisa. Panaitaji kazi ya wataalamu katika sekta ya barabara watendaji fanyeni kazi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...