image004 (8)
Mtaalamu wa masuala ya vyombo vya habari jamii na Mkufunzi Bi Rose Haji Mwalimu (aliyesimama) wakati wa ufunguzi kijiji cha Usagara, wilayani Misungwi mkoani Mwanza hivi karibuni.

Na Modewjiblog team, Mwanza
Tabia ya watu kukwepa kutoa ushahidi mahakamani ni sababu mojawapo ya wahalifu wa mauaji ya albino kutotiwa hatiani na kuachiwa huru.

Hayo yameelezwa katika warsha zilizoendeshwa mfululizo wilayani Misungwi, Kahama na Bariadi za ushirikishwaji wa jamii katika kuzuia na kutokomeza ukatili, unyanyasaji na unyanyapaa kwa watu wenye ulemavu wa ngozi (albinism) nchini.

Wakichangia mada kuhusu changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu wa ngozi, washiriki wamesema kwamba imekuwa ni kawaida kwa watu kutokuwa tayari kutoa ushahidi mara wanapoitwa mahakamani kwa sababu zisizokuwa na mashiko.

Sababu hizo ni kuogopa kuuawa na wahusika na shinikizo kutoka kwa wanafamilia.
“Mara nyingi tumeshuhudia watu wanaoitwa mahakamani kutoa ushahidi hawaendi siku kesi inaposikilizwa hata kama aliandikiwa na mahakama kufanya hivyo, wengine huamua kuhama kabisa eneo analoishi kwa kukwepa lawama kutoka kwa jamii au familia na kuogopa kuuawa baada ya kugundulika kuwa katoa ushahidi,” alisema mmoja wa washiriki.

Kuachiwa kwa watuhumiwa wanaodaiwa kuhusika na ukatili hususan kukatwa viungo na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi kumezua mjadala mkubwa katika jamii kwamba jeshi la polisi haliwajibiki kikamilifu au kuhisiwa kuwa na ushirikiano wa namna fulani na watuhumiwa hao.
DSC_0577
Afisa mtetezi na ushawishi kutoka shirika linaloshughulika na watu wenye Albinism la Under The Same Sun (UTSS), Kondo Seif akisisitiza jambo kwa washiriki katika warsha ya siku tatu iliyofanyika katika kijiji cha Nyakasungwa wilayani Sengerema mkoani Mwanza hivi karibuni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...