wafanyakazi wa Hoteli ya Dar es Salaam Serena ambao ni wakereketwa wakubwa wa mazingira, waliadhimisha siku hii asubuhi ya leo kwa kufanya usafi barabara ya Ohio kuzunguka mpaka ufukwe wa bahari ya Hindi.

Akiongea  mara baada ya zoezi hilo la usafi mkurugenzi mkuu wa masoko wa hoteli hiyo ndugu Seraphin Lusala aliwashukuru wafanyakazi wa hoteli hiyo kwa kushiriki katika zoezi hilo la kufanya usafi wa mazingira ili kuonyesha mfano kwa jamii kwamba uchafuzi wa mazingira haukubaliki na kuwataka wafanyakazi wa hoteli hiyo kuwa mfano hata huko wanapoishi kwa kutokutupa taka hovyo na kuwaelimisha wale wanaotupa taka hovyo na kuchafua mazingira kuacha tabia hiyo ili kufanya mazingira yetu na jiji letu kuwa safi.
 wafanyakazi wa Hoteli ya Dar es Salaam Serena ambao ni wakereketwa wakubwa wa mazingira wakiendelea na zoezi la usafi kando ya barabara ya Ocean Road, jijini Dar katika kuadhimisha siku ya Mazingira.
wafanyakazi wa Hoteli ya Dar es Salaam Serena ambao ni wakereketwa wakubwa wa mazingira wakiwa katika picha ya pamoja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...