Na. Catherine Sungura, MOHSW-Arusha

Zaidi ya wagonjwa elfu arobaini wanaougua ugonjwa wa vikope unaotokana na trakoma wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa macho katika mikoa sita nchini Tanzania kwa muda wa miaka mitano.

Hayo yamezungumzwa jana jijini hapa na Mratibu wa Mpango wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele dkt. Upendo Mwingira wakati akiwasilisha mada kwenye mkutano wa nne wa kazi kati ya wizara na wadau wanaofadhili mpango huo Upasuaji huo unafadhiliwa na shirika la msaada la Uingereza (DFID) pamoja na mfuko wa msaada wa Malkia Elizabeth (QETF) katika mikoa ya Mtwara, Lindi, Arusha, Manyara, Pwani pamoja na Dodoma.

Dkt. Mwingira alisema tathimini iliyofanyika nchi nzima inakadiriwa kuwa na wagonjwa wa vikope wapatao laki moja, hivyo ili kudhibiti ongezeko la upofu nchini ,serikali imeanza kufanya upasuaji wa wagonjwa hao.

“Watu wenye matatizo ya vikope hupata usumbufu wakati kope zikigusa kioo cha jicho na mwishowe kupofuka,hivyo njia hii ya upasuaji itawasaidia kurudi katika hali ya kawaida na kujisaidia katika shughuli zao binafsi na zile za maendeleo ya Taifa kwa ujumla” alisema Ugonjwa wa vikope husababishwa na bakteria aina ya “Chlamydia Trachomatis” wanaosambazwa na inzi na pia kwa njia ya kuchangia taulo au vitambaa na kugusa macho ya mtu anayeugua ugonjwa huo , hivyo usipotibiwa mapema unaweza kusababisha upofu.

Mkutano huo unawajumlisha wadau kutoka nchini Washington DC, Liverpool, Geneva pamoja na baadhi ya waratibu wa mpango huo toka mikoa ya Tanzania bara.
Dkt.Upendo Mwingira akimkabidhi zawadi ya kinyago mwakilishi mkazi wa shirika la IMA World Health Jim Cox anayemaliza muda wake nchini.IMA World Health ni moja ya wadau wa mpango huo.
Dkt. Jeremiah Ngondi kutoka RTI International ambayo inatekeleza Mpango wa Taifa Kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele, akizungumza katika Mkutano huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...