IDADI kubwa ya waimbaji  wa nyimbo za Injili Tanzania wameonesha nia ya kumsindikiza mwenzao, Bonny Mwaitege anayetarajia kuzindua albamu yake Agosti 2 mwaka huu.

Uzinduzi huo unaotarajia kufanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam ambao utashirikisha albamu tatu za muimbaji huyo zinazoendelea kurekodiwa jijini Mwanza.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama hivi sasa utaratibu wa kurekodi albamu hizo unaendelea jijini Mwanza. Msama aliyezungumza na Mwandishi wa gazeti hili jijini Mwanza alisema amepokea maombi ya waimbaji mbalimbali hapa nchini ambao wanahitaji kuwa pamoja na mwenzao huyo.

Msama alisema kwa kuwa bado wanaendelea na hatua za mwisho za kufanikisha kazi hizo, wanajipanga kushirikisha idadi kubwa ya waimbaji watakaomsindikiza mwezao. Aidha Msama alisema sambamba na waimbaji hao kutaka kupanda jukwaani siku hiyo, pia mashabiki wa muziki huo hapa nchini wanahitaji uzinduzi wa albamu hiyo ushirikishe pia waimbaji raia wa Afrika ya Kusini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...