MAHAKAMA YA TANZANIA YAKUTANA NA UJUMBE KUTOKA BENKI YA DUNIA PAMOJA NA WADAU WENGINE WA MAHAKAMA KUJADILI JUU YA MABORESHO YA HUDUMA YA UTOAJI HAKI NCHINI
Mhe. Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Tanzania (katikati), Mhe. Shaaban Ali Lila, Jaji Kiongozi  wa Mahakama Kuu ya Tanzania (wa tatu kulia), Bw. Waleed Malik, Mtaalam kutoka BENKI ya Dunia, (wa tatu kushoto), Mhe. Adel Kent, Jaji kutoka Mahakama Canada  (wa pili kushoto), Bw. Menbere kutoka Mahakama-Ethiopia (wa pili kulia), Mhe. Hussein Kattanga, Mtendaji Mkuu Mahakama ya Tanzania, ( wa kwanza kulia) na Mhe. Ignas Kitusi, Msajili Mkuu Mahakama ya Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja na Wawakilishi kutoka Benki ya Dunia na baadhi ya Majaji wa Mahakama ya Tanzania waliosimama Mara baada ya ufunguzi wa Warsha Kati ya Mahakama na Benki ya Dunia na Wadau wengine wa Mahakama, warsha hiyo imelenga katika kuangalia Kuhusu uboreshaji wa huduma za  Mahakama na jinsi ya kusogeza huduma za Mahakama karibu na wananchi.
 Meza Kuu ikiwa katika picha ya pamoja na wadau wa Mahakama kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Chuo cha Sheria, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, na baadhi ya Wawakilishi kutoka REPOA na wengineo walioshiriki katika Warsha kati ya Mahakama, Ujumbe wa Benki ya Dunia na Wadau wa Utoaji haki juu ya uboreshaji wa utoaji huduma za Mahakama na kusogeza huduma za Mahakama karibu na wananchi.
 Mhe. John Kahyoza, Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania akitoa mada juu ya Maboresho yanayoendelea kufanyika ndani ya Mahakama ya Tanzania kwa washiriki wa Warsha hiyo.
Washiriki wa Warsha hiyo wakisikiliza mada inayotolewa juu ya Maboresho ya Mahakama, moja Kati ya maeneo yaliyojadiliwa katika kuleta maboresho ni pamoja na Kurahisisha upatikanaji wa haki, kuboresha utawala wa Mahakama, kuimarisha Imani ya wananchi kwa Mahakama, na Ushirikishwaji wa wadau katika kuboresha huduma za Mahakama. (Picha na Mahakama ya Tanzania).






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...