Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angellah Kairuki akisisitiza namna mabaraza ya ardhi yanavyopaswa kufanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa, wakati wa mkutano wa Waziri wa wizara hiyo  na wananchi wa kata ya Makongo leo jijini Dar es salaam. Katikati ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi na wa kwanza kushoto ni Diwani wa Kata ya Makongo Deusdedith Mtiro.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni Yusuph Mwenda akimshukuru Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi na ujumbe wake kwa kuahidi na kusisitiza kuwa kufanikiwa kwa mradi wa Makongo kutahamasisha mpango wa ushirikishwaji wa wananchi katika kuendeleza ardhi na kuwa na makazi bora ambapo kufanikiwa kwake kutahamasisha mpango huo kutekelezwa maeneo mengine ndani ya Manispaa ya Kinondoni.
 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi na akiongea na wananchi wa Kata ya Makongo Manispaa ya Kinondoni (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam juu ya Mpango Shirikishi wa kuendeleza ardhi na makazi ya wananchi kwa kushirikiana na Serikali.
 Mkazi wa Makongo juu Bi Ritha Mbotto akimuuliza swali Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi (hayupo pichani) wakati mkutano na wanchi wa kata ya Makongo Manispaa ya Kinondoni leo jijini Dar es salaam. Kushoto ni mwandishi wa habari wa TBC Edward Kondela.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...