Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Bi. Beng’i Issa (kulia) pamoja na Rais wa Cambridge Development Initiative (CDI), Bw. Ravi Solanki wakitia saini makubaliano ya kuimarisha elimu ya ujasiriamali kwa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini jana jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia ni Afisa Mwandamizi wa uwekezaji, NEEC, Bw. Oswald Karadisi (kulia) na Mkurugenzi Ujasiriamali wa CDI, Bi. Georgia Ware.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Bi. Beng’i Issa (kulia) akipongezana na Rais wa Cambridge Development Initiative (CDI), Bw. Ravi Solanki (kushoto) baada ya kutia saini makubaliano ya kuimarisha elimu ya ujasiriamali kwa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini jana jijini Dar es Salaam. katikati ni Mkurugenzi wa Ujasiriamali wa CDI, Bi. Georgia Ware.

Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam

Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) limefikia makubaliano na Cambridge Development Initiative (CDI) ili kuimarisha mafunzo ya maswala ya ujasiriamali kwa wanafunzi wa vyuo vikuu hapa nchini.

CDI ni mpango ulioasisiwa na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Cambridge cha nchini uingereza ambapo wanafunzi wenye vipaji toka chuo hicho na vyuo vikuu hapa nchini wanakutana, kubadilishana uzoefu ili kutatua changamoto mbalimbali.

Mkataba wa makubaliano hayo umetiwa saini na Katibu Mtendaji wa NEEC, Bi. Beng’i Issa wakati Rais wa mpango huo, Bw. Ravi Solanki aliwakilisha wenzake.

Akiongea na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam baada ya kutia saini mkataba huo, Bi. Beng’i alisema elimu na maarifa ya ujasiriamali ni muhimu sana kwa sasa ambapo changamoto ya ajira ni kubwa dunia nzima, Tanzania ikiwa mojawapo.

“Mzingatie sana maarifa mnayopata hapa…yatawasaidia katika maisha yenu,” aliwaasa wanafunzi hao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...