Makamu wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Wallace Karia ametuma salama za pongezi kwa uongozi mpya wa klabu ya Coastal Union uliochaguliwa mwishoni mwa wiki.

Katika salamu zake kwa Mwenyekiti mpya wa klabu hiyo Dr. Twaha, Karia amesema anawapa pongezi wa kuchaguliwa na kupewa heshima hiyo na wanachama wa Coastal Union katika kuitumikia klabu yao.

“Kikubwa wanachopaswa kufanya kwa sasa ni kuodokana na makundi ya aina yoyote, na kuifanya Coastal Union kuwa kitu kimoja na kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom” alisema Karia.

Aidha Karia amesema, TFF itashirkiana na uongozi mpya katika utendaji wa kazi na kuleta maendeleo katika mpira miguu nchini.

Klabu ya Coastal Union yenye makazi yake jijini Tanga ilifanya uchaguzi wake mwishoni mwa wiki na kuwapata viongozi wake wapya, akiwemo mwenyekiti, makamu mwenyekiti na wajumbe wa Kamati ya Utendaji.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...