Baraza
la Sanaa la Taifa (BASATA) ambalo ni msimamizi wa sekta ya Sanaa nchini
linawakumbusha wasanii wote nchini kuhakikisha wanafuata sheria, kanuni
na taratibu zilizopo wanapokwenda nje ya nchi kufanya maonesho au
kushiriki shughuli yoyote ya Sanaa ili kuepuka matatizo na mikanganyiko
mbalimbali inayoweza kujitokeza.
Kwa mujibu wa taratibu zilizopo, msanii yeyote anapokwenda nje ya nchi anapaswa kujaza fomu maalumu inayotolewa na BASATA na baadaye kupewa kibali bure (bila gharama yoyote) ambacho mbali na kueleza wapi msanii anaelekea kinaeleza kwa kina tarehe ya kuondoka kwa msanii na ile ya kurudi nchini.
Kutokana na kukua kwa sekta ya Sanaa nchini hususan muziki na filamu wasanii wengi wamekuwa wakipata fursa ya kwenda nje ya nchi kufanya maonesho na shughuli zingine za Sanaa hivyo suala la kufuata sheria, kanuni na taratizu za kupata vibali vya kwenda nje ya nchi ni muhimu sana ili kuhakikisha kwanza; safari zao zinakuwa na baraka ya moja kwa moja kutoka Serikalini, pili kusaidia upatikanaji wa takwimu sahihi za wasaniii wanaokwenda nje ya nchi, tatu usalama wa wasanii wetu na mwisho, kuwakabidhi bendera ya taifa kama ishara ya uwakilishi na ubalozi wa nchi yetu katika mataifa wanayoyatembelea.
Kwa mujibu wa taratibu zilizopo, msanii yeyote anapokwenda nje ya nchi anapaswa kujaza fomu maalumu inayotolewa na BASATA na baadaye kupewa kibali bure (bila gharama yoyote) ambacho mbali na kueleza wapi msanii anaelekea kinaeleza kwa kina tarehe ya kuondoka kwa msanii na ile ya kurudi nchini.
Kutokana na kukua kwa sekta ya Sanaa nchini hususan muziki na filamu wasanii wengi wamekuwa wakipata fursa ya kwenda nje ya nchi kufanya maonesho na shughuli zingine za Sanaa hivyo suala la kufuata sheria, kanuni na taratizu za kupata vibali vya kwenda nje ya nchi ni muhimu sana ili kuhakikisha kwanza; safari zao zinakuwa na baraka ya moja kwa moja kutoka Serikalini, pili kusaidia upatikanaji wa takwimu sahihi za wasaniii wanaokwenda nje ya nchi, tatu usalama wa wasanii wetu na mwisho, kuwakabidhi bendera ya taifa kama ishara ya uwakilishi na ubalozi wa nchi yetu katika mataifa wanayoyatembelea.
Basata mkajipange upya, sababu zenu bado zina utata mkubwa tu
ReplyDeleteSIASA ZA BASATA..NASEEB ABDUL KAWAUMBUA SANA
ReplyDeleteKama msanii anaenda huko nje kwa gharama zake kwa nini apitie kwenu?
ReplyDeleteAcheni sanaa iwe soko huria mambo ya ukiritimba "msanii apate Baraka toka Basata" yamepitwa na wakati.